Kijana leo
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 2,861
- 810
Habari humu ndani,
kwa wataalamu naomba mnisaidie, ninapata maumivu ya kichwa makali sana na kupelekea macho kuuma sana, hata nikigeuka au kuinama ili nipate kujisikia nafuu mpaka nifumbe macho. Kwa anayefahamu tatizo ni nini? na tiba yake ni nini? asanteni na usiku mwema.
cc: mzizi mkavu, Dr mo.
Maumivu ya Kichwa
Chukua unga wa Habbat-Sawdaa kipimo cha vijiko 3 kikubwa cha kulia wali ,na karafuu iliosagwa nusu ya kiwango cha Habbat-Sawdaa na Anisuni (anise) kijiko kimoja na nusu , halafu Uchanganye
pamoja. Uchukue kiasi cha kijiko kimoja (cha chai), wakati wa kuumwa na kichwa, na Unywe na maziwa lala (mala), na Unga mwengine wa kupasugua
mahala panapo uma kwa mafuta ya Habbat-Sawdaa .huo unga changanya na hayo mafuta ya Habbat-Sawdaa ujisugue.
Kama upo Mjini Dar nenda kaulize wanaouza dawa za kiarabu wapemba karibu na sokoni kariakoo utapata hiyo Habbat sawdaa unautwanga na kuuchekecha uwe unga.Huo unga wa habbat sawdaa ndio unga gan na unapatikana wapi?