maonesho linatokana na ona, onesha: fanya kitu kionekane
maonyesho linatokana na onya; kumrekebisha mtu aliyekosea, kumtia adabu, kumtahadharisha na hatari fulani.
*lakini kwa sababu lugha hubadilika kutokana na kupita kwa wakati pamoja na mazingira, watu hutumia maonyesho kumaanisha maonesho.
Tofauti kati ya nadhani/nazani, dhambi/zambi, thelathini/selasini, themanini/semanini, tafadhali/tafadhali, tofauti zote hizo husababishwa na mazingira au watu kutozingatia sana sheria za lugha. Kuna watu wengi wana tatizo na matamshi yenye, "dh", na "th".
Kuna msemo wa kiswahili, "mazoea hujenga tabia"