Msaada wadau juu ya TOEFL

Msaada wadau juu ya TOEFL

Mbavu za Mbwa

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2011
Posts
303
Reaction score
154
Ndugu zangu,
Kwa anayefahamu vizuri, utaratibu wa kufanya hii mitihani ya TOEFL(Test Of English As a Foreign Language) naomba anielekeze katika nukta hizi:-

(i) Kwa hapa Tanzania vituo vya mitihani vipo mikoa ipi?

(ii) Usajili hufanyika kipindi gani na mitihani hufanyika kipindi kipi?

(iii) Usomaji wake ukoje?

(iv) Ada yake ni bei gani? Kama ni ada ya masomo/mtihani

(v) Ufafanuzi mwingine wowote ambao ni relevant na mitihani hii ya TOEFL

Shukrani
 
Kama upo dar mimi nafahamu kituo kipo IST international school of tanganyika masaki..nenda hapo kaulizie upate maelekezo kama upo mikoani tafuta international schools..za ukweli zenye IGCSE au american system of education sio uchwara upate maelekezo..over..!!
 
Pia unaweza fika British council hapo Dar, kama unaruhusiwa kufanya other English language test apart from TOEFL, mie nilifanyia hapo na wanatoa training ya maandalizi ya huo mtihani. na CD za kumwaga na material yakutosha. Na utapewa information zaidi. Otherwise panda online search web site yao utapata more information.
 
Mkuu nakushauri upie IELTS Pale british council. Ina modules 4 ambazo ni speaking ,listening ,reading na writting.
Ada yake nadhan itakuwa kwenye laki 5. Mi nlifanya iyo test 2010 na nlilipa laki 3 kwa wakat ule.
Kama unaswali uliza
 
Kuna jengo Moja opposite na CBE nenda pale kuna mama wa kihindi anafundisha vizuri sana unalipia Kama dola 70 hivi utapata skills zote na atakupa pia CD's na current books. Ufanye mwenyewe mazoezi na hakika Kama huna taabu sana na lugha basi 2 weeks zinatosha na utafanya vizuri. Mitihani nakushauri ufanye UCC UDSM
 
Nashukuruni sana ndugu zangu. Mi nipo mikoani, inabidi nifanye mchakato. Thanks much
 
Back
Top Bottom