Msaada wakuu nakoroma hadi kero

baba mausingizi

Senior Member
Joined
Jun 15, 2016
Posts
189
Reaction score
119
Wadau mwenye ufahamu kwenye hili tatizo,nakoroma sana nikilala na hali hii siipendi sinywi pombe,siyo mnene,ila tatizo linanitesa kuna dawa au njia yoyote kupunguza tatizo hili pls nipo serious
 
Miye ninalo hilo tatizo nilishajaribu njia nyingi mfano kuachama na kusukuma ulimi nje mara kadhaa lakini tatizo haliishi, wakati mwingine huwa naogopa hata kulala wakati wenzengu bado hawajalala kuepuka kuwakela
 
Mimi nilisumbuliwa miaka mingi sana,na nilipitia kipindi ambacho kilinitesa sana.

Kipind napangiwa O level kwenda kusoma hapo ndio ukawa mtihani kwangu nitaenda kuishi vipi,maaana nilikuwa nakoroma kama SIMBA.

Nilikutana na jamaa mmoja akaniambia ili upone tatizo hili lakupasa ulale KIFUDIFUDI.

Alinisisitizia ni zoezi gumu sana kama mtu hukuzoea kulala hivyo,ila kama unataka kupona basi lala hivyo.

Sikuwa na jinsi na lengo lilikuwa kupona,basi nikaanza kulala hivyo lakini nilipitia changamoto kubwa sana,yaani unashangaa umegeuka na kuanza kukoroma.

Basi ikawa tunashinda nikigeuka na kwasababu ukikoroma huwa unasikia mwenyewe naamka haraka na kulala KIFUDIFUDI.

Mpaka leo hui nimezoea na kipindi narud likizo nyumban walistaajabu kuona SIKOROMI KABISA nipo walipokuwa wananiuliza ni nani aliokupa hii dawa.


NB:MKUU JARIBU KULALA KIFUDIFUDI UTAFANIKIWA KABISA.
Wadau mwenye ufahamu kwenye hili tatizo,nakoroma sana nikilala na hali hii siipendi sinywi pombe,siyo mnene,ila tatizo linanitesa kuna dawa au njia yoyote kupunguza tatizo hili pls nipo serious
 
Ukikoroma unajisikia? Utakuwa haujalala wewe
 
Miye ninalo hilo tatizo nilishajaribu njia nyingi mfano kuachama na kusukuma ulimi nje mara kadhaa lakini tatizo haliishi, wakati mwingine huwa naogopa hata kulala wakati wenzengu bado hawajalala kuepuka kuwakela
Ni kero tena ukiwa ugenini ndo kabisa
 
Asante mkuu ngoja nijaribu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…