Msaada wakuu!!!!

Kamuone T.B.Joshua akufanyie maombi ya deliverence
 
Mkuu umejibu vema kabisa, suwala la jinamizi halina uhusiano wowote na nguvu za Giza wala Kiza na kuondoka kwake hakuna uhusiano wowote wa kumkabidhi maisha yako mtu yoyote yule zaidi ya wewe mwenyewe.

Kama kama quote hiyo hapo juu inavyo jieleza na wale wengine waliojaribu kuchangia kunako fanana na hayo maelezo. Hali ya kuhisi kukabwa usingizini ni matokeo ya ulalaji m'baya na haswa utokea unapolala chali na wakati mwingine inawezekana unalala ukiwa umeshiba sana na hii upelekea kuongezeka kwa kitu kinachoitwa body's metabolism na ambayo usababisha ubongo wako kujishughulisha sana, na kupelekea kupata Jinamizi...!

Vile vile Jinamizi usababishwa pale unapokuwa na msongo wa mawazo (stress and anxiety). Wataalam wa ndoto na hisia wanasema kuwa Jinamizi au Nightmare umpata mtu kwa muda kuanzia dakika tano (5) mpaka ishirini (20). Na mara nyingi uendana na mtu kulia au kutoa miguno hafifu...!

Kama umelala na mwenzako na kuona hali hii basi unatakiwa kumuamsha kwa kumtikisa kidogo kidogo au kwa kumnyanyua kuanzia usawa wa kifua, hii itamsaidia mlengwa kama Jinamizi lake linatokana na shibe basi itapelekea matumbo yake (abdominal cavity) kurudi katika nafasi yake na kuacha kukandamiza diaphragm ambayo inatenganisha mapafu na matumbo ya ndani (abdominal cavity).

Kwa tatizo lako ili unatakiwa kuzingatia mambo haya yafuatayo:

Usilale hali ya kuwa umeshiba sana, wacha nafasi kwenye tumbo lako kwa vitu vitatu, Mosi nafasi ya chakula, Pili nafasi ya maji na Tatu nafasi ya wewe kuweza kupumua vizuri.

Kuna msemo mmoja upo hivi:

"Eat BREAKFAST like a King, LUNCH like a Prince, and DINNER like a Beggar"

It means that... Breakfast should be rich foods, Lunch should be Heavy foods, and the Dinner should be very lighter foods.

Vile vile unatakiwa kupunguza mawazo na wasiwasi unapokuwa unataka kulala, hii itakusaidiakuepukana na kuota ndoto za ajabu ajabu kama vile ngono n.k.
 

well said x-paster now i understood and i'm going to overcome the problem.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…