Msaada waungwana: Biashara ya uwekezaji kupitia DSE

bhikola

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,131
Reaction score
1,663
Habari wanajamii.
Nimekuwa na shauku kubwa sana ya kuwekeza katika amana na dhamana hasa za serikali. Lakini nimekuwa nikipigwa danadana na watu wa kati ambao ni CRDB Bank.

Mwezi Januari nilitaka kununu dhamana. Nikamtumia mtu huyu wa kati maana nipo mkoani ambapo brokers wengine hawapo. Lakini kila wakati amekuwa akiniambia kuwa sishindi minada.

Sasa nashindwa kuelewa sishindi minada vipi? Akasema naweka bei ndogo. Nikaamua kuweka bei ya Tshs 100 kwa kila Tshs 100. Bado nikaambiwa sishindi. Hapa ndipo nilipogundua kuwa nahujumiwa.

Sasa nimeamua kumtafuta broker mwingine. Lakini changamoto ni kwamba, akaunti ya uwekezaji niliyofungua wanayo CRDB na hawataki kunipa jina na no za akaunti hiyo.

Nimejaribu kuwaandikia DSE kupitia ki barua pepe walichoweka pale kwenye tovuti yao nao hawataki kunijibu malalamiko yangu.

Nashindwa kuelewa, hamtaki watanzania tuwekeze kupitia hilo soko lenu au ni kitu gani hiki? Na je, Malalamiko yangu niyapeleke wapi?

Asanteni
Kama kuna sehemu inahitaji maelezo zaidi nipo tayari kueleza ili nisaidiwe
 
Nadhani ufafanue zaidi, hawakupi acc no kivipi? Ulipofungua hiyo account haukupata details za account yako?

Kuuza na kununua shares lazima kuwe na pande mbili kama unaweka bei ndogo au bei iliyo sawa na bei ya sasa ya hisa labda unaweza kukosa muuzaji, pia kama bonds ni mnada na kuna wanaoweka dau kubwa zaidi yako unaweza ukakosa. Pia labda idadi unayotaka kununua inaweza ikawa inaleta tatizo kama ni kiasi kidogo ambacho hakileti commission ya kutosha.

Labda uongee vizuri na broker wako akupe details ya hizo bonds/shares zinauza kwa bei gani ili uweke dau sahihi.
 
Mara zote nimewekeza huku sijawahi kuulizwa na broker kiasi ninacho weka, huwa nawaambia jumla kiasi gani ninacho, wanaenda sokoni, wakirudi wananiambia tumefanikiwa kupata Kwa kiasi gani. Sijawahi kufikiria kwa nini hawanihusishi kwa hilo, labda kuna la kujifunza hapa. Lakini mara zote majibu yakitoka naweza nisiwe na minimum Accepted bid lakini huwa siwi mbali sana. Kuhusu namba ya akaunti, nimeshatumia broker zaidi ya mmoja na sijawahi kumpa yoyote kati yao namba kutoka kwa mwingine.
 

Mkuu naweza kujifunza kitu hapa.
Sasa inakuwaje kwa upande wangu? maana kwamfano Solomon Brokers wanasema mpaka niwape a/c hiyo iliyofunguliwa na CRDB ndo waweze kununua.
Sasa nishauri ndugu, nafanyaje kutatua changamoto hii?
 

Asante mkuu,
Mimi nachotaka kununua ni bonds na siyo shares.
Kununua bonds, minimum amount ni laki tano. kwahiyo ukiwa na kuanzia kiasi hicho, unaruhusiwa kununua. Na kumbuka commission huwa haizidi 2% ya kiwango unachowekeza.
Kwenye kutenda hizi bonds, unakuwa unanunua kila Tshs 100. yaani kwa mfano unasema, bond ya shs 100 nitainunua kwa shs 95. kwa maana hiyo hakuna bid ya zaidi ya shs 100 hiyohiyo. Hauwezi kununua shs 100 kwa shs 110.
Ukitaka kuwekeza kwenye dhamana za serekale, lazima ufungue acc ya uwekezaji Benki Kuu. acc hii inaita BOT-CDS account. sasa hii account ndo nimeshafungua lakini details zake ndo imeshindikana kuzipata.
natumaini nimejieleza vya kutosha
asante
 
Mkuu naweza kujifunza kitu hapa.
Sasa inakuwaje kwa upande wangu? maana kwamfano Solomon Brokers wanasema mpaka niwape a/c hiyo iliyofunguliwa na CRDB ndo waweze kununua.
Sasa nishauri ndugu, nafanyaje kutatua changamoto hii?
Nenda kwa broker kama mteja mpya wakufungulie account labda kama utaratibu umebadilika. Hata sasa sijui kama natumia account moja au tofauti kila broker na wake.
 
Nenda kwa broker kama mteja mpya wakufungulie account labda kama utaratibu umebadilika. Hata sasa sijui kama natumia account moja au tofauti kila broker na wake.

Thanks bro/sisy let me try this oprion
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…