Msaada wenu mnaofahamu vizuri suala hili

uzeebusara

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2013
Posts
657
Reaction score
514
Kuna mdogo wangu alimaliza kidato chat sita comb PCB with addition of two subjects BAM and GS. Matokeo yake alipata diivision 3 ya point 12 ambapo alipigwa penati ya kufeli BAM na GS. Sasa maswali yako Hivi:
1. Anaomba kufahamishwa utaratibu wa kuyarudia masomo hayo ya BAM na GS kama inawezekana.
2. Je cheti chake baada ya kurudia kitakuwa ni division 2 au division 3 iwapo atakuwa amefaulu masomo hayo?
3. Kama ni hivyo kituo Kipi ni kizuri ajiandikishe yupo hapa Dar es salaam, Sinza ambapo atapata wepesi wa materials na walimu wa kumsaidia gharama sio tatizo.
4. Je hajachelewa kufanya mtihani mwaka huu?

Msaada wenu Wanajamvi
 
Je kwa nini arudie mtihani? Ninavyojua, ili kuendelea na Elimu ya juu inahitaji ufaulu wa masomo matatu yanayounda mchepuo. Au je, kanuni zimebadikia siku hizi. Nasema hivyo kwa kuwa kuna watu walifeli GS na BAM, ila walifaulu vizuri masomo ya msingi kwa principla pass, na sasa wapo vyuo vikuu. Hata kama hakufaulu Kidato cha Sita, ufaulu wa Kidato cha Nne, hususani hesabu, unazingatiwa.
Naomba ufafanuzi hapo, ili nijue pa kuanzia kukushauri.
 

Asante mkuu kwa maswali yako. Kwa suala la kanuni hata mimi binafsi Sijui kwa sasa kama ni zilizile tulizotumia miaka hiyo ya zamani au la. Pili huyu mdogo wangu ktk masomo yake ya principles kapata flat Ds kwenye PCB. Nia yake ni asome udaktari wa binadamu ss alienda kwa lecturer mmoja akamshauri afanye tena mitihani hy ya hayo masomo ya BAM na GS, kwa hl hata mimi sijajua nia ya yule mkuu kumwambia studies mitihani hy ni kuwa asafishe cheti na kuongezea nafasi zaidi ya kuchaguliwa au la hl Sijui. Ss kutokana na hali hy bs dogo kaja wangu wangu hataki llt kwanza mpk afanikiwe suala hl na mm binafsi sina ufahamu wa mambo haya nikaona nitupe kwenu kwa hl ni jukwaa la weledi.
 
Division 3 point 12 kama sikosei atakuwa na principal zaidi ya moja na sikuhizi vyuo vinapokea hata ukiwa 4.5 sasa huyu ndg yako anasubiri nini mpaka sasa hapo nyumbani? kwa nn asiombe udaili Tcu anawaza maswala ya kurudia mtihani.
 

Fuata habari za usahihi TCU!! Bila kukosea, kwa mtu anayetaka kusomea udaktari anapaswa kuwa na cut-off points 3.5, ikiwa kama ana D tatu (ina maana ana principal 3) ambazo zina uzito wa cut-off points 6.
Kwa uhakika zaidi, tembelea mtandao wa TCU ( www.tcu.go.tz ), kisha angalia masharti ya kujiunga na kozi mbalimbali mwaka wa masomo 2013/14. Tayari wameshatoa mwongozo. Tena fanya haraka kwa kuwa mmwisho wa mwezi huu ndio wanafunga nafasi kwa waombaji waliohitimu miaka ya nyuma.
Kwa bahati mbaya huwa tunapata hasara kubwa maishani kwa kukosa maarifa na washauri sahihi, hususani baada ya kupata habari kutoak kwa watu wasohusika.
 
Hata kama hajakidhi vigezo vya kusomea shahada, mshauri asome Stashahada. Mshauri aache kudharau (kama anadharau Stashahada). Kuna vyo kadhaa, hususani vya binafsi, vinavyotambulika na kutegemewa na serikali kuandaa wataalamu wa afya.
Amini nakuambia, kurudia mtihani ni uwekezaji wa hatari kuwahi kufikiriwa kufanywa na huyo ndugu yako, na kama atafeli jamii nzima ya watu wanomzunguka watakuwa wamefeli kumshauri vyema (labda agomee ushauri).
 

Asante Mkuu kwa mwongozo wako. Nafanyia kazi. MOLA akuzidishie hekima na busara
 
aombe udahili achaneni na kurudia mtihani wkt mtu amefaulu, akikosa, wapo walioenda na dv 3 za kawaida. Fanya mpango uende chuo, kwa sabab bado anasafar ndefu kufaulu huo udocta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…