Msaada wenu tafadhali

Msaada wenu tafadhali

Mshobaa

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2013
Posts
1,714
Reaction score
677
Kwanza nianze kwa kutanguliza heshima mbele yenu, nina mdogo wangu ambaye huwa anasumbuliwa sana na kifua tangu akiwa na 2age mpaka sasa ana 12 age na bado tatizo linaonekana bado kuwa sugu kwani tumeshajaribu dawa karibia zote kwenye mahospitali na hakuna mafanikio yeyote, huwa anashinda vizuri ila ikifika saa moja jioni huwa anabanwa mpaka kupumua inakuwa ni tabu huku akikoroma kwa kuambatana na maumivu makali kifuani. Ombi langu kwenu kwa mwenye ufahamu wowote tafadhali tusaidiane kwa moyo mmoja... Dr Mzizi mkavu popote ulipo msaada wako hapa jamvini
 
Mkuu mimi =tumejitahidi kumpima lakini wanasema hana pumu na huwa wanatupa tu dawa kuwa zitamsaidia lakini bado ndugu yangu ni mtihani
 
Last edited by a moderator:
Pole, ..Uzito wake na urefu ni upi?
Lakini unaposema ana tatizo la kifua una maanisha nini? ...anapumua haraka, anapumua kawaida ila kwa shida, ana pata maumivu kifuani, anakohoa au tatizo hasa ni lipi?

Tatozo hili humpata mara ngapi kwa siku/wiki/mwezi? Hutokea hasa wakati gani wa siku mf asb/mchana/usk? wakati gani wa majira ta mwaka wakati wa masika/kipupwe n.k! Je kuna dawa zozote kati ya zile alizowahi kutumia ziliwahi kumpa unafuu? Zipi? Tofauti na kifua je, mtoto husumbuliwa na harufu ya marashi, baadhi ya viungo!!

Vipi tatizo la kutokwa jasho jingi, mikono (hasa vidole vya miguu kubadilika na kuwa kama rangi ya blue), choo chake kikoje (kilicho laini sana)?Kuna mtu katika familia/ukoo mwenye tatizo kama hilo?
 
Asante mkuu, hippocratessocrates, huwa anakohoa mpaka muda mwingine pumzi zinakuwa ni kwa shida na huwa analalamika maumivu kifuani na wakati anakohoa huwa kama kuna makohozi mazito na humtokea kwa muda wa lisaa limoja na mwisho huwa anatema makohozi mazito na hapo anapata nafuu kabisa na usiku huo huwa anakoroma mpaka asubuhi na hali hiyo huwa inaendelea wiki nzima, tatizo hili huwa linatokea kila mwezi ikifika kwenye tar 20 kwa miezi yote 12, huwa tatizo hili linamtokea kila ikifika mida ya jioni na mchana huwa anashinda bila tatizo lolote, dawa za hospitali huwa mara nyingi hazionyeshi dalili yeyote na huwa tunampatia asali iliyochanganywa na asali huwa inampa nafuu sana, huwa hasumbuliwi na tatizo lolote la harufu, huwa hatoki jasho kama ulivyoainisha hapo wala kubadilika rangi,na kwenye ukoo na wala familia hakuna mtu aliyekuwa/ analo hilo tatizo.ni hayo mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Dawa ya Kifuwa ya Tiba Mbadala chukuwa kitungu Maji 1 kimenye na ukikate vipande 4 , uweke katika kijiko kikubwa kimoja cha Asali fresh funika vizuri uweke pembeni ikae usiku mpaka kesho yake itatowa maji ,, kama syrup basi mpe kijiko kimoja mara tatu au mara 4 kwa siku inshaallah itamsaidia. tumia kwa muda wa siku 3 au siku 7 kisha uje hapa unipe feedback.@Mshomba
 
Dawa ya Kifuwa ya Tiba Mbadala chukuwa kitungu Maji 1 kimenye na ukikate vipande 4 , uweke katika kijiko kikubwa kimoja cha Asali fresh funika vizuri uweke pembeni ikae usiku mpaka kesho yake itatowa maji ,, kama syrup basi mpe kijiko kimoja mara tatu au mara 4 kwa siku inshaallah itamsaidia. tumia kwa muda wa siku 3 au siku 7 kisha uje hapa unipe feedback.@Mshomba

thanks bro ngoja tujaribu kaka
 
Dawa ya Kifuwa ya Tiba Mbadala chukuwa kitungu Maji 1 kimenye na ukikate vipande 4 , uweke katika kijiko kikubwa kimoja cha Asali fresh funika vizuri uweke pembeni ikae usiku mpaka kesho yake itatowa maji ,, kama syrup basi mpe kijiko kimoja mara tatu au mara 4 kwa siku inshaallah itamsaidia. tumia kwa muda wa siku 3 au siku 7 kisha uje hapa unipe feedback.@Mshomba

Safi sana
Tiba mbadala ndo uhalisia wenyewe

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom