Msafiri Kafiri au Kakiri?

Msafiri Kafiri au Kakiri?

KOKUTONA

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2011
Posts
8,651
Reaction score
6,104
Hodi humu.
Juzi nilikuwa kwenye dala dala, na ilikuwa imejaa sana. Bahati mbaya mkaka mmoja alimkanyaga mdada kwa bahati mbaya. Yule mdada akaja juu kweli, lakini yule mkaka akajishusha akaseme na kumuomba radhi yule mdada. Nanukuu "Samahani dada, sikudhamiria kukukanyaga, pole sana. Ndo hivyo tena MSAFIRI KAFIRI"

Mara watu waaanza kunong'ona chini chini, akatokea mdada mmoja akasema "Kaka unatuharibia lugha bwana hakuna kitu kama,msafiri kafiri ni MSAFIRI KAKIRI"

Yalianza mabishano ya pande mbili, yaani wanaoamini kuwa sahihi ni msafiri kafiri na wanaojua sahihi ni msafiri kakiri.

Nilishuka mabishano yakiwa yanaendelea, na habari ya dada kukanyagwa iliyeyuka ghafla.

Wataalam wa lugha naomba kujuzwa, ipi ni sahihi? Kwa uelewa wangu siku zote nilikuwa najua msafiri kafiri, hii kakiri ilikuwa mpya kwangu.

Nawasilisha
 
Mimi najua hivyo hivyo...kafiri, unaruhusiwa vitu ambavyo kikawaida haviruhusiwi. kama kuchimba dawa njiani, kula nyama ya mbwa au kibudu na mengineyo.
 
Hodi humu.
Juzi nilikuwa kwenye dala dala, na ilikuwa imejaa sana. Bahati mbaya mkaka mmoja alimkanyaga mdada kwa bahati mbaya. Yule mdada akaja juu kweli, lakini yule mkaka akajishusha akaseme na kumuomba radhi yule mdada. Nanukuu "Samahani dada, sikudhamiria kukukanyaga, pole sana. Ndo hivyo tena MSAFIRI KAFIRI"

Mara watu waaanza kunong'ona chini chini, akatokea mdada mmoja akasema "Kaka unatuharibia lugha bwana hakuna kitu kama,msafiri kafiri ni MSAFIRI KAKIRI"

Yalianza mabishano ya pande mbili, yaani wanaoamini kuwa sahihi ni msafiri kafiri na wanaojua sahihi ni msafiri kakiri.

Nilishuka mabishano yakiwa yanaendelea, na habari ya dada kukanyagwa iliyeyuka ghafla.

Wataalam wa lugha naomba kujuzwa, ipi ni sahihi? Kwa uelewa wangu siku zote nilikuwa najua msafiri kafiri, hii kakiri ilikuwa mpya kwangu.

Nawasilisha
Ni msafiri Kakiri,kukiri ni kukubali maana yake msafiri kakubaliana na lolote lile akiwa safarini liwe la kheri au shari
 
Ni msafiri Kakiri,kukiri ni kukubali maana yake msafiri kakubaliana na lolote lile akiwa safarini liwe la kheri au shari

Labda kwa lugha nyingine, lakini kwa Kiswahili usahihi ni "Msafiri Kafiri". Na haina mantiki mtu kukiri kitu au jambo ambalo halijatokea.
 
Hodi humu.
Juzi nilikuwa kwenye dala dala, na ilikuwa imejaa sana. Bahati mbaya mkaka mmoja alimkanyaga mdada kwa bahati mbaya. Yule mdada akaja juu kweli, lakini yule mkaka akajishusha akaseme na kumuomba radhi yule mdada. Nanukuu "Samahani dada, sikudhamiria kukukanyaga, pole sana. Ndo hivyo tena MSAFIRI KAFIRI"

Mara watu waaanza kunong'ona chini chini, akatokea mdada mmoja akasema "Kaka unatuharibia lugha bwana hakuna kitu kama,msafiri kafiri ni MSAFIRI KAKIRI"

Yalianza mabishano ya pande mbili, yaani wanaoamini kuwa sahihi ni msafiri kafiri na wanaojua sahihi ni msafiri kakiri.

Nilishuka mabishano yakiwa yanaendelea, na habari ya dada kukanyagwa iliyeyuka ghafla.

Wataalam wa lugha naomba kujuzwa, ipi ni sahihi? Kwa uelewa wangu siku zote nilikuwa najua msafiri kafiri, hii kakiri ilikuwa mpya kwangu.

Nawasilisha
Msafiri Kakiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom