Msanii Mack T amerudi kwa kishindo

mpenda pombe

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
1,406
Reaction score
711
Leo nimebahatika sikiliza wimbo mpya wa msanii mkongwe Mike T Clouds FM, unaitwa umenikutaga, hakika jamaa karudi vizuri Sana na wimbo wake utasumbua Sana.

Nikiwa Kama shabiki wazamani wa nguli huyu, nampongeza kwa kazi Hii nzuri na Classic chini ya upishi wa Maco Chali.
 
Mkuu Mike T wa sasa sio yule wa zamani hiyo ngoma haitomfikisha popote kwani ipo kawaida sana.Hebu tujikumbushe hizi hit songs za mnyalu miaka ile;
1.Nampenda ft. Nature
2.Nyaluland ft.Jide
3.Nibeep
4.Kama
5.Sintobadilika ft Q Chillah
6.Sintobadilika remix ft. Dully Sykes
 

Nakubaliana nawe, ila kwa ngoma Hii ni jiwe kwa wakati huu.. Tukiupa muda huu wimbo naamini unafika mbali.
 
Umesahau Je Utanipenda, idea iliyorudiwa na Diamond
 
Hapakuwahi kuwa na msanii maarufu wa muziki kwa jina la Mack T hapa Tanzania
 
Hiyo namba 4 kama unayo pls iweke hapa....Ni bonge moja la Ngoma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…