Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,916
- 43,505
Ukisikiliza huu wimbo toka mwanzo utapata maana ye neno mashine kwenye huu wimbo,Katika Wimbo wake kila mara nimesikia akitaja ' mafanikio ' mengi ya Mwanaume ila kila mara anasisitiza tu kuwa Mwanaume ' Mashine '. Sisi wengine ni ' Wageni ' katika nchi hii na hatukijui vizuri Kiswahili hiki cha Kitanzania hasa hiki cha ' Pwani ' hivyo nawaombeni sana Watanzania na ' Waswahili ' mliotukuka mnisaidie kuniambia Msanii Msaga Sumu hapa alipokuwa akiimbia kwa kusema " Sifa ya Mwanaume Mashine....Mwanaume Mashine....Mwanaume Mashineeeeeeeee...." anamaanisha nini?
Nawasilisha.
Mwanzo anasema mwanaume sio sura mwanaume ni kuchapa kazi, mwanaume kujituma.... mwanaume ni mashine..
Hapo ana maanisha mwanaume anatakiwa kufanya kazi kama mashine(kuchapa kazi,kujituma)