Niache Nteseke
JF-Expert Member
- Apr 29, 2020
- 2,162
- 2,616
Msanii maarufu wa Ukraine anayejulikana kwa jina la Pasha amefariki Dunia kutokana na kushambuliwa kwa makombora na wavamizi wa Urusi huko Irpin, Ukraine.
Kifo cha msanii huyo kiliripotiwa na mwanasheria na mwandishi wa habari Yaroslav Kuts.
"Hawakuwa na hata wakati wa kupiga picha ambazo walikusudia kuzipiga, kwa kifupi nnachoweza kusema ni.....Rest in peace Pasha," aliandika kwenye account yake ya Facebook.
Wakati wa kifo cha Pasha, alikuwa na umri wa miaka 33 tu. Msanii huyo alijiunga na sanaa miaka mingi iliyopita. Katika muda wa saa 48 zilizopita, kumekuwa na fursa ya kuketi na kutupa picha kuhusu jinsi wanavyopigwa na mabomu lakini bado walikuwa wanatabasamu, kwa sababu waliweza kukabiliana nayo, na kila kitu kingebaki kwa Ukraine. Kwa kifupi tunafanya kazi !". Hiko ndicho alichoandika muigizaji huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram.