Awsom
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,085
- 307
Nimefanya kazi na wasanii kwa kipindi kirefu kidogo.
Ninajua wazi kuwa hakuna wakati ambapo muziki na sanaa umetambulika kama ajira, biashara na fani rasmi katika sekta za kiuchumi kama katika serikali awamu ya nne. Tumetoka mbali na changamoto kubwa bado zipo zifanyiwe kazi.
Muziki na sanaa hivi sasa vinamchango mkubwa kwenye GDP.
Mnyonge mnyongeni lkn haki yake mpeni.
Wasanii wetu wakubwa wa level ya Ray wananyonywa ni kwa sababu ya kubweteka na kusubiri kila kitu kiletwe na serikali. Mtu anasubiri serikali isimamie mauzo ya kazi zake, kumtafutia soko na kufanya mikataba.. wengi hawajifunzi na kutumia njia ka kisasa za usimamizi wa kazi zao na biashara zao kama lilivyo kwa makampuni..ingekuwa biashara zingine za sekta binafsi zinaendeshwa hivyo tungeshahama mji siku nyingi.
Sheria za intellectual property zishaendelea sana siku hizi. Na kuna fursa kibao zinazotokana na technolojia ya kisasa amabayo haitumiki kabisa.
Mkuu unachosema ni sahihi kwamba wasanii wanatakiwa watumie oportunity zilizopo kuuza kazi zao,kama vile internet na kutafuta masoko nje ya TZ,ila usiseme kuwa wanabweteka kwasababu hizo Ahadi ni serikali peke yake ndiyo iliyoahidi.
Sidhani kama kuna msanii aliwahi kuadress kwa serikali suala la kujengewa classic studio. Vilevile wasanii wanavyolalamikaga kuhusu kazi zao kusambazwa mitaani kila mara ni Serikali iliahidi kushuhulikia hilo.Neither step nor follow up towards that issue has been taken seriously. Kwahiyo Ray anajua anacholalamikia.