msanii wa bongofleva Barnaba Aonyesha Mkoko wake mpya..!!

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
Bado huamini kwamba muziki wa bongo sasa unalipa? Kama umejibu ndiyo nakushauri u-update fikra zako sababu wasanii wa miaka ya sasa wamekuwa wakionesha mafanikio ya aina mbalimbali yanayotokana na kazi ya muziki wanayoifanya.

Barnaba wa THT leo amemwonesha ‘baby wake’ mpya kupitia Instagram, tena akiwa bado hata hajapewa ‘birth certificate’.

Ameionesha gari yake mpya aina ya Toyota Mark X ikiwa bado na chasis namba na kuandika “Oyeaaaaa Thanx Lod imetimia”.


Katika picha nyingine Barnaba a.k.a baba Steve aliandika “New”, na picha ya tatu aliandika “Kaz nzuri na mambo mazuri”.

 
Yaani mark x nayo ni mafanikio?!
Aisee! Bora kwend shule. Somesheni watoto jamani

Kweli upo sawa,
Huwezi sema mziki unalipa kwa kununua mark x while umeimba miaka nenda rudi. Aachane na mziki hauna issue kwake.
 
Wana JF acheni nirudi kwny fani yng ya kuimba soon nita make head line umu jukwaani chezea mm afu nanunua vitz mpyaaaaaaaaa.....!
 
hongera zake, pia ametokelezea sana pichani
 
Barnaba rudi shule elimu yako ya muungano primary baada ya miaka 10 haitakusaidia
 
Well....sijui alikuwa na gari gani au kama ana gari nyingine ila kwa maoni yangu alipaswa awe na mafanikio zaidi ya hii gari (huenda anayo, hapa hatujui vizuri). Kama sio, wasanii kweli wananyonywa
 
Barnaba rudi shule elimu yako ya muungano primary baada ya miaka 10 haitakusaidia

siku hizi elimu yenyewe haisaidii kukuweka juu kimaisha.kinachosaidia ni unafanya nini?

watu wanalalamika hawana ajira, mshahara mdogo wakati kuna msanii show moja analipwa million 10.

Barnaba japo hajasoma lakin amewazidi wengi kimaendeleo ata wenye masters.

siyo kila mtu anatoka kimaisha kwa kusoma. cha muhimu aweke bidii kaz anayofanya pia ajifunze ujasiriamali. hizi elimu zetu hazisaidii zaidi ya kufundisha mtu ili akimaliza akazulule kutafuta kazi
 
Money Stunna hivi huyu brother ana house? Kama ameshajenga music unalipa...
 
Last edited by a moderator:

Hujanielewa
 
Tatizo la wasanii wa bongo wanahangaika na present Hulu future wameiweka mfuko wa nyuma c ajab baada ya miaka 5 ukaskia hali yke ya ki uchumi ni tete anaomba msaada
 
Money Stunna hivi huyu brother ana house? Kama ameshajenga music unalipa...

Kama nyumba hana amepanga apo itakua majanga lakin kama kajenga ndo tunaitaga ndo maisha safi maisha huwa ni nyumba vingine mbwee mbwee so kama vyote anavyo ajitulize na mkee wake wajenge maisha?
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…