Msanii wa vichekesho, Joti jitathmini katika hili

Msanii wa vichekesho, Joti jitathmini katika hili

Shujaa Nduna

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2022
Posts
599
Reaction score
487
Nimeangalia clip yake ya maigizo inayoitwa(kazi na ngono)katika igizo hili limeanza vema lakini ktk kumaliza nadhani lina utata. Joti aliigiza kama binti mwenye elimu ya digrii anayetafuta kazi, lakini bosi akamtaka kimapenzi ili ampe kazi na aliposhindwa kugawa uroda bosi hakumpa kazi.

Joti akarudi nyumbani na kumsimulia mama yake na hatimaye yeye mama na mtoto wakaambatana kwenda ofisini. Na walipofika ofisini mama akamkamata roba bosi na kutoka naye nje halafu Joti akakalia kiti cha bosi ofisini na kuanza kutumia desk top kama mfanyakazi.

Sasa kwanini nasema amekosea, igizo lilipoanza lilikuwa linaashiria kufundisha kupinga unyanyasaji wa kingono toka kwa mabosi, rushwa ya mapenzi. Lakini limeisha kwa kuteka ofisi. Watalam mnisaidie hii ni sawa ktk kuwasilisha ujumbe?
 
Mbona hakutekwa yule jamaa katolewa ofisini tu anatekwaje mtu kwa kelele hiyo tena ndani ya ofisi yake mwenyewe na wafanyakazi wakiwemo?
 
Nimeangalia clip yake ya maigizo inayoitwa(kazi na ngono)katika igizo hili limeanza vema lakini ktk kumaliza nadhani lina utata. Joti aliigiza kama binti mwenye elimu ya digrii anayetafuta kazi, lakini bosi akamtaka kimapenzi ili ampe kazi na aliposhindwa kugawa uroda bosi hakumpa kazi.

Joti akarudi nyumbani na kumsimulia mama yake na hatimaye yeye mama na mtoto wakaambatana kwenda ofisini. Na walipofika ofisini mama akamkamata roba bosi na kutoka naye nje halafu Joti akakalia kiti cha bosi ofisini na kuanza kutumia desk top kama mfanyakazi.

Sasa kwanini nasema amekosea, igizo lilipoanza lilikuwa linaashiria kufundisha kupinga unyanyasaji wa kingono toka kwa mabosi, rushwa ya mapenzi. Lakini limeisha kwa kuteka ofisi. Watalam mnisaidie hii ni sawa ktk kuwasilisha ujumbe?
Tamthilia za BONGO Maigizo yasiyo na Tija na Uhalisia mengi sana
 
Nimeangalia clip yake ya maigizo inayoitwa(kazi na ngono)katika igizo hili limeanza vema lakini ktk kumaliza nadhani lina utata. Joti aliigiza kama binti mwenye elimu ya digrii anayetafuta kazi, lakini bosi akamtaka kimapenzi ili ampe kazi na aliposhindwa kugawa uroda bosi hakumpa kazi.

Joti akarudi nyumbani na kumsimulia mama yake na hatimaye yeye mama na mtoto wakaambatana kwenda ofisini. Na walipofika ofisini mama akamkamata roba bosi na kutoka naye nje halafu Joti akakalia kiti cha bosi ofisini na kuanza kutumia desk top kama mfanyakazi.

Sasa kwanini nasema amekosea, igizo lilipoanza lilikuwa linaashiria kufundisha kupinga unyanyasaji wa kingono toka kwa mabosi, rushwa ya mapenzi. Lakini limeisha kwa kuteka ofisi. Watalam mnisaidie hii ni sawa ktk kuwasilisha ujumbe?

huo ndio usaniii wa bongo huwa ni wa ovyoo kabisa
 
Acha kukaza fuvu hukuona secretary na pale si ofisini
Nadhani huelewi namna ya uwasilishaji. sekretari alikuwa chumba kingine sekretari hakai na boc chumba kimoja.Pia igizo lilivyoanza na lilivyoisha ni sawa?Hapo ndipo penye hoja kuu usiambuliye kucheka tu.
 
mleta mada una ubongo uliosinyaa sana.

Kwanza hujui kutafsiri kazi ya sanaa.
Pili nampongeza joti kwa kuleta conflict kwenye namna ya upokeaji ambapo ni kazi nzuri ya sanaa kumchanganya mpokeaji wa kazi ile.
Tatu heb fanya kazi mwenzako ashaingiza siku ww ndo kwanza unaleta malalamiko jf kwan hao youtube na media zinazoonyesha hawajachambua kwakajua kua inamafundisho au haina.
 
Kwani Huna jambo lolote lile la kuwaza linaloweza ongeza hicho kipato chako kiduchu?

Joti anatumia nguvu nyingi kufosi talent, mpuuzie.
 
Nadhani huelewi namna ya uwasilishaji. sekretari alikuwa chumba kingine sekretari hakai na boc chumba kimoja.Pia igizo lilivyoanza na lilivyoisha ni sawa?Hapo ndipo penye hoja kuu usiambuliye kucheka tu.
Haya bhana mzee wa BASATA
 
Ile ni kazi ya kisanaa, sanaa kazi yake nyingine ni kuacha mafumbo ili mtazamaji atumie akili yake kutafsiri mafumbo hayo.
Joti kaonyesha kuwa chochote kinaweza kumtokea bosi kama hatozingatia miiko ya kazi yake, Bosi kupinduliwa katika ofisi yake ni kama kutumbuliwa tu, na yeyeote akisimamia wajibu wake anaweza kumpindua bosi wa aina kama yake.
 
Bora hata wale wanaojadili kula tunda kimasihara kuliko wewe mtoa mada
 
Mkuu ulitaka afanyaje? Mbona wengine wanaimba rakatarakata reketerekete rukuturukutu na Bado wanalipa mkuu?
 
Unateseka na vitu vidogo sana mkuu, hiyo ni sanaa
 
Ushasema ni msanii wa Vichekesho hayo mengine kwake ni ziada...

By the way kuwa Critic sio Mbaya inaruhusiwa kwenye haya mambo ila una-criticize kazi na sio mtu mambo ya kujitathmini hapo unavuka mipaka tukianza kuwapangia kazi wasanii sio poa cha maana wewe tunga yako ambayo mwisho wake ni kama unavyotaka wewe
 
Back
Top Bottom