Msemaji Mkuu wa Serikali: Tumerudisha Bilioni 9 za Bureau De Change

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
“Serikali imesharudisha takribani TZS bilioni 9 kwa wafanyabiashara waliokuwa wamewekeza kwenye Bureau de Change [maduka ya kubadili fedha] ambazo zilikuwa zimekamatwa katika oparesheni iliyofanyika, na baada ya kujiridhisha na kukuta wamefuata na kuzingatia vigezo, wamerudishiwa fedha zao ili waendelee kufanya mambo yao.” – Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa


View: https://www.instagram.com/p/CwaEGr6KTTp/
 
Msemaji Alitakiwa Aachie Ngazi chap Chap
Maana Alikuwa Na Jiwe Wakati Yanafanyika Hayo
 
Zimerudishwa kwa kina nani sasa?

Siasa za hovyo sana nchi hii na kuna wapuuzi wataamini!
 
Mh 🤔 means ilikua ni uporaji au wivu wa kimaendeleo?
 
Atoe uthibitisho vinginevyo ni porojo kama nyingine
 
Hapo ukute hela wamejichotea tu na kusingizia wamerudisha kwa walio pokonywa, Namama yetu alivyo kuwa kilaza basi ni taabu tupu yeye anadhani kunyamaza ndiyo suluhisho.
 
Serikali ya mwenda zake ilifanya unyang'anyi na wizi mkubwa sana. Miaka waliyoua bihashara za watu hao pasina faida watawafidia wafanyabihashara hao?
 
Bandari vipi mtarudisha kwa watanzania ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…