Msemaji wa Simba SC Haji Manara nakuheshimu na nakukubali sana ila kwa hili la wana Simba SC Kuishangilia Yanga SC tuombe radhi.

Msemaji wa Simba SC Haji Manara nakuheshimu na nakukubali sana ila kwa hili la wana Simba SC Kuishangilia Yanga SC tuombe radhi.

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Ole wake nimuone mwana Simba SC yoyote yule Uwanjani anaishangilia Yanga SC hasa katika Michuano yake ya Kimataifa. Simba SC tutazishangilia Azam FC na KMC pekee ila kwa Yanga SC watatusamehe kwani hata Wazee Wetu wa Simba SC walioko Makaburini sasa wakisikia eri Mashabiki wa Simba SC wanaishangilia Yanga SC nadhani Watatulaani vibaya mno kwani Kwetu hili ni mwiko kabisa.

Binafsi hata nikiona Yanga SC inacheza Mechi ya Timu inaitwa Matapishi FC Mimi nitaishangilia hiyo Timu mwanzo mwisho na kamwe iwe mchana au usiku siwezi na sitothubutu kuja Kuishangilia Yanga SC hata nishawishiwe vipi na nani hilo ni gumu.

Haji Manara ( Msemaji Wetu Simba SC ) acha Kututafuta ubaya tafadhali halafu tukakuchenjia na Wewe. au unatulazimisha tuishangilie Yanga SC kwakuwa Baba yako Mzazi ni mwana Yanga SC lia lia? Hivi kwa akili yako kabisa unadhani kuna mwana Simba SC Mpumbavu atakuja Kuishangilia Yanga SC hata Siku moja?

Na kama ni Ustaarabu Kwao Simba SC ndiyo tuliuanza miaka ile ya 90 lakini cha Kushangaza katika ile Mechi ya Fainali ya Simba SC na Asec Abidjan kama siyo Stella pale Shamba la Bibi ambapo Boli Zozo alitutungua Goli 2 nzuri tu mwanzoni wana Yanga SC walikuwa wanatushangilia Simba SC ila tulipofungwa tu hizo Goli wakaanza Kutuimba ule Wimbo wao ambao hadi leo unaniuma ukisema ..." Uzalendo Umetushinda....Uzalendo Umetushinda....Uzalendo Umetushinda ".

Ukitaka nigombane nawe au nikuchomolee Betri ya Teja nitajie Yanga SC. Siwapendi na sitokuja Kuwapenda kamwe na daima.

Haiwezekani.
 
Wote mnaoshangalia timu za nje muwe ni mashabiki wa Yanga, Simba, takataka gani sijui! huwa nawaona hamnazo kabisa kichwani. Mniwie tu radhi.

Binafsi ni shabiki wa Yanga, lakini inapotokea Simba ikacheza na timu ya nje, ni ukweli ulio wazi! nitafarijika kuiona Simba ikishinda. Utaifa kwanza halafu utani wetu ubakie pale tu tunapocheza wenyewe kwa wenyewe.
 
Wote mnaoshangalia timu za nje muwe ni mashabiki wa Yanga, Simba, takataka gani sijui! huwa nawaona hamnazo kabisa kichwani. Mniwie tu radhi.

Binafsi ni shabiki wa Yanga, lakini inapotokea Simba ikacheza na timu ya nje, ni ukweli ulio wazi! nitafarijika kuiona Simba ikishinda. Utaifa kwanza halafu utani wetu ubakie pale tu tunapocheza wenyewe kwa wenyewe.
Kweli kabisa Muungwana umezungumza.
Kushangilia timu ya nje inapocheza na timu ya ndani ya nchi yetu ni tatizo.
Na nadhani halizuiliki kwani Kuna baadhi ya watu Wana matatizo ya Kisaikolojia, hao wanaoshangilia timu za nje.
 
In
Haiwezekani.
Inawezekana, labda kwako wewe, na wengine wanao ona kushabikia mpinzani wake wa kimichezo ni dhambi na kamwe haiwezi tokea. Tubadilike, sie wote ni Watanzania, Kimataifa tupeane support "inapowezekana", Tubadilike watanzania ushabiki wa Usimba na Uyanga Uwe kwa Ligi za ndani ya inchi tu.

Mkuu An Eagle Usije chana chana jezi za Yanga maana umeonesha hasira na huipendi yanga (Wanayanga) toka moyoni (Simba Nguvu Moja)
 
Wote mnaoshangalia timu za nje muwe ni mashabiki wa Yanga, Simba, takataka gani sijui! huwa nawaona hamnazo kabisa kichwani. Mniwie tu radhi.

Binafsi ni shabiki wa Yanga, lakini inapotokea Simba ikacheza na timu ya nje, ni ukweli ulio wazi! nitafarijika kuiona Simba ikishinda. Utaifa kwanza halafu utani wetu ubakie pale tu tunapocheza wenyewe kwa wenyewe.

Unapotushangaa Sisi tunaoshangilia Timu za nje mbona hujishangai na Wewe ambaye Kutwa unatizama tu Tamthilia na Michezo ya Kuigiza ya Ulaya au Nigeria huku za hapa Kwako Tanzania ukizipuuza kama siyo Kuzidharau? Acha Unafiki tafadhali. Hujawahi Kuona Mzazi anampenda sana Mtoto wa Jirani ila wake anamchukia? Umeshajiuliza ni kwanini? Hivi Wapenzi wa Tanzania ni wao tu pekee ndiyo Washamba na hawana Akili kama ulivyotuita hapa kwakuwa wanashangilia Timu za Nje ila za hapa hawazishangilii? Unataka kusema kuwa hakuna Wahispania au Wajerumani au Wafaransa au Wamarekani au Wachina ambao nao wanazishangilia sana Timu na Ligi Kuu Kipenzi ya Uingereza?

Una uwezo mdogo / finyu wa Kujenga Hoja ( kwa Lugha nyepesi hapa namaanisha kuwa Wewe ni Kichwa Maji ) kabisa. Mbona ukiwa na Demu wako unakimbilia kununua Condoms za Ulaya na hizi zako za Mikocheni unazikimbia na huzitumii? Je hapa na Wewe unakuwa siyo Mpumbavu / Kichwa Maji?

Nimekudharau mno!
 
In

Inawezekana, labda kwako wewe, na wengine wanao ona kushabikia mpinzani wake wa kimichezo ni dhambi na kamwe haiwezi tokea. Tubadilike, sie wote ni Watanzania, Kimataifa tupeane support "inapowezekana", Tubadilike watanzania ushabiki wa Usimba na Uyanga Uwe kwa Ligi za ndani ya inchi tu.

Mkuu An Eagle Usije chana chana jezi za Yanga maana umeonesha hasira na huipendi yanga (Wanayanga) toka moyoni (Simba Nguvu Moja)

Nina Hasira nao kweli hao Yanga SC na hasa hasa Kocha wao Mpuuzi Zahera na Yule Mshambuliaji wao Miss Bantu Molinga.
 
kushabikia yanga ni kukosa vitamin Fulani kichwani, waliyoyafanywa mwaka jana ACL hakuna namna tutaungana nao; wacha Township Rollers tuwape maujanja na wamalize kazi huko kwao, tuliwapa hapa tz sasa kazi ni kwao huko kwao
 
Unapotushangaa Sisi tunaoshangilia Timu za nje mbona hujishangai na Wewe ambaye Kutwa unatizama tu Tamthilia na Michezo ya Kuigiza ya Ulaya au Nigeria huku za hapa Kwako Tanzania ukizipuuza kama siyo Kuzidharau? Acha Unafiki tafadhali. Hujawahi Kuona Mzazi anampenda sana Mtoto wa Jirani ila wake anamchukia? Umeshajiuliza ni kwanini? Hivi Wapenzi wa Tanzania ni wao tu pekee ndiyo Washamba na hawana Akili kama ulivyotuita hapa kwakuwa wanashangilia Timu za Nje ila za hapa hawazishangilii? Unataka kusema kuwa hakuna Wahispania au Wajerumani au Wafaransa au Wamarekani au Wachina ambao nao wanazishangilia sana Timu na Ligi Kuu Kipenzi ya Uingereza?

Una uwezo mdogo / finyu wa Kujenga Hoja ( kwa Lugha nyepesi hapa namaanisha kuwa Wewe ni Kichwa Maji ) kabisa. Mbona ukiwa na Demu wako unakimbilia kununua Condoms za Ulaya na hizi zako za Mikocheni unazikimbia na huzitumii? Je hapa na Wewe unakuwa siyo Mpumbavu / Kichwa Maji?

Nimekudharau mno!

Msimamo wangu uko pale pale! Uwe Yanga au uwe Simba, utakapoamua kuishangilia Ud Songo kwa sababu tu inacheza na Simba Taifa, au ukaishangilia Township Rollers kisa tu inacheza na Yanga Taifa; huo ni wendawazimu!

Nitaishabikia Kagera Sugar ikicheza na Simba! lakini Simba hiyo hiyo ikicheza na Ud Songo, nitaishabikia Simba kwa maslahi ya Taifa! na huo ndiyo ushabiki na utani wa jadi wa kweli. Kuhusu kushabikia timu za nje, hilo siyo tatizo. Hata mimi ni shabiki wa Real Madrid ya Spain na pia ni shabiki wa Chelsea ya Uingereza! Kwa hiyo usichanganye nilichokielezea awali.

Kuhusu bongo muvi, chonde chonde! washauri tu wabadilike. Waache kurahisisha muvi zao. Kwa sasa wacha niendelee kuangalia Korean Drama za akina Jumong, na wengineo.
 
Haji Manara hakusema tuishangilie Yanga.Alisema tusiwazomee wala kushangilia timu pinzani. Kwa hilo namuunga mkono.Alisema kama hatuwezi kuacha kuzomea tubaki nyumbani.
 
Haji Manara hakusema tuishangilie Yanga.Alisema tusiwazomee wala kushangilia timu pinzani. Kwa hilo namuunga mkono.Alisema kama hatuwezi kuacha kuzomea tubaki nyumbani.

Mtoa mada kuna kitu ambacho siyo cha kawaida atakua amefanyiwa na Yanga! Maana anatokwa na mapovu kiasi mpaka unashangaa. Na anataka watanzania wote wafuate msimamo wake hata kama hauna tija kwa maslahi mapana ya Taifa.
 
Mtu unaempa sapot na yeye anakupa sapot?.. Hapo ndio shida ilipo.
Soka la nchi hii napenda kama Taifa tuendelee kupeleka timu 4 katika mashindano ya CAF kama wenzetu CONGO, ZAMBIA n.k... Hii itafanya Klabu kama MTIBWA, KMC, LIPULI, KAGERA, MBAO n.k wapambane zaidi kupata nafasi za juu hata FA CUP.
In'short ligi yetu ushindani utaongezeka zaidi ya hapa ulipo sasa... Na timu zitajengwa kwa ustadi mkubwa ili zikashindane.
Kuhusu kuacha kuzomeana ni kitu ambacho kimeota sugu hapa kwetu.. Sababu ya UTANI na USHABIKI uliokomaa ambao hakuna dawa yake hata TAMKO ATOE RAIS itaonekana maigizo tu.
Cha msingi timu zilizo kwenye CCL + CONF Zitambue Ushindi ndio huvuta mashabiki kwanza.. Kama wanatambua hilo basi hakuna haja ya kuzozana sana sisi mashabiki, wanaozomea huwezi kuwaona kama timu inashinda, wakomae na sapot wanayopata inawatosha.
Huwezi kushangiliwa na wote, hakuna mechi ya upande mmoja.
 
Mtu unaempa sapot na yeye anakupa sapot?.. Hapo ndio shida ilipo.
Soka la nchi hii napenda kama Taifa tuendelee kupeleka timu 4 katika mashindano ya CAF kama wenzetu CONGO, ZAMBIA n.k... Hii itafanya Klabu kama MTIBWA, KMC, LIPULI, KAGERA, MBAO n.k wapambane zaidi kupata nafasi za juu hata FA CUP.
In'short ligi yetu ushindani utaongezeka zaidi ya hapa ulipo sasa... Na timu zitajengwa kwa ustadi mkubwa ili zikashindane.
Kuhusu kuacha kuzomeana ni kitu ambacho kimeota sugu hapa kwetu.. Sababu ya UTANI na USHABIKI uliokomaa ambao hakuna dawa yake hata TAMKO ATOE RAIS itaonekana maigizo tu.
Cha msingi timu zilizo kwenye CCL + CONF Zitambue Ushindi ndio huvuta mashabiki kwanza.. Kama wanatambua hilo basi hakuna haja ya kuzozana sana sisi mashabiki, wanaozomea huwezi kuwaona kama timu inashinda, wakomae na sapot wanayopata inawatosha.
Huwezi kushangiliwa na wote, hakuna mechi ya upande mmoja.

Hakuna Kuishangaila Yanga SC bali wajishangilie wenyewe. Nimemaliza.
 
manara kashangilie yanga yeye na baba yake sisi simba ambao tumekuwa washabiki wa muda mrefu kamwe hatutaishangilia yanga manara kaja simba juzijuzi na kujifanya anatujua sana mashabiki wa simbaa
 
Nawashangaa watu wazima mnavyodanganyana, uzalendo kwenye mpira haupo popote pale duniani, Arsenal na Spurs hawawezi ishangilia Chelsea hata siku moja labda matokeo yawe yanafaida kwao, vile vile kwa Barcelona na Madrid, City kwa United, kwenye mpira mafanikio yako ndio rungu la kumcheka mwenzio, hivyo Simba hawez shangilia Yanga, na Yanga hawezi shangilia Simba, mengine yote ni unafiki tu
 
Back
Top Bottom