Hivi ni zeruzeru au zeluzelu? N ways vyovyote vile jamaa ni hivyohivyo!Kwani Haji siyo zeluzelu? Kwani tukisema kocha wa yanga na simba ni wazungu tumewakashifu? Hata mkimtetea vipi atabaki kuwa zeluzelu milele
Wekeni na maneno ya Manara yaliyomfanya Bumbuli atamke maneno hayoKuna clip inasikika ambayo, msemaji wa Yanga ndugu H.Bumbuli anamporomoshea matusi makubwa na kumdhalilisha msemaji wa Simba ndugu Haji Manara!
Amesikika akimkebehi kwa kuwa alibino, na kutoa maneno ambayo kiukweli hayafai katika jamii!
Huyu Bumbuli alifanywa kitu na Manara kiasi cha kumporomoshea matusi mazito hivyo Manara..!?
Kama ni masuala ya mpira tu, hata kama ni mambo mengine, amekosea sana!
Mpira siyo uhasama, kuwa watani wa jadi siyo kutukanana na kudhalishana!
...Bumbuli, anafaa achukuliwe hatua stahiki ili iwe fundisho!
Hata na hivyo Haji Manara amekuwa mstaarabu na kusema kuwa anamsamehe kwa aliyoyafanya! Hiki alichofanya Haji ni ustaarabu lakini, hili linaweza kujitokeza tena kwa mwingine na ikawa ni mazoea kudhalilishana ama kutukanana kisa mambo ya mpira, ambao kwa kweli ni burudani kwa walio wengi!
Hiyo clip najaribu kuipandisha inagima hapa!
Naamini wapo wenye hiyo clip, ila pitia hapa utaweza kuiona!
Hivi, tujiulize matusi si alitukanwa Manara !!! Sisi tumejuaje kama katukanwa?Hebu tuwekeni ushabiki wa Simba na Yanga pembeni. Kiukweli Bumbuli amekosea sana namna alivyomtukana Manara na hasa lile tusi alilotukana watu wenye ulemavu wa ngozi. Kuacha ulemavu ambao mtu anazaliwa nao, mtu yoyote anayejiona mzima sasa hivi anaweza kupata ulemavu wakati wowote na ndio maana kuna msemo usemao sisi wote ni walemavu watarajiwa. Kwa hiyo Kwa hali yoyote ile yale matusi ya Bumbuli hayakubaliki hata kidogo katika jamii iliyostaarabika.
Lakini tumejiuliza huyu Manara aliyetukanwa na Bumbuli ni msafi kiasi gani? Tusi lile lile Manara alilotukanwa na Bumbuli (sipendi kulitaja) ndilo Manara amemtukana Jerry Muro juzi juzi tu hapa, amemtukana sana Antoni Nugaz na ndilo alilomtukana sana Tshishimbi mwaka mmoja au miwili hivi iliyopita kwenye page yake ya Instagram. Vipi yeye kurudishiwa kidogo na Bumbuli tu anaanza kutafuta huruma kwenye vyombo vya habari na kusahau kuwa hata Jerry Muro, Antonio Nugaz na Tshishimbi nao ni binadamu na wanahisia na maumivu kama yeye Manara anayoyapata sasa. Tusiwatendee wenzetu kile ambacho sisi wenyewe tukitendewa tunashindwa kuvumilia na pia tukumbuke kipimo tunachowapimia wenzetu ndicho hicho hicho tutapimiwa na sisi kama sio leo basi tutapimiwa kesho.
Kwenu Bumbuli na Manara mmebeba dhamana kubwa sana. Tambueni kuwa Simba na Yanga ni taasisi kubwa sana Tanzania zinafuatiliwa na mamilioni ya watanzania kuanzia watoto, vijana,wazee, maaskofu, mashehe, mapadri, makuli, mama ntilie, wagema mnazi, wabeba zege, wakulima n.k. bila kujali umri, jinsia, itikadi za siasa au dini kwa hiyo chochote mnachokifanya au kukiongea kwenye vyombo vya habari tumieni weledi na busara zaidi badala ya kutumia mihemuko.
Michezo ni furaha. Tubishane kuhusu Simba na Yanga bila kuwatukana au kuwakwaza wenzetu. Mwisho wa siku nyinyi Manara na Bumbuli ni binadamu na ni watanzania nje ya Simba na Yanga mnazozifanyia kazi na kuzishabikia. Hamtadumu milele mkiwa wasemaji wa Simba na Yanga na ipo siku itafika mtakuwa nje ya hizo timu mkiwa aidha mmetimuliwa au mmeacha kazi wenyewe. Je, mmeshajiuliza itakuwaje baada ya kuondoka kwenye hivyo vilabu na mtakuwa mmeacha "legacy" gani?