Msemo wa "kama kawaida" wazua tafrani

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
37,630
Reaction score
47,434
Jamaa alikuwa mteja wa kitimoto eneo flani wakati dini yake hairuhusu.

Siku ya siku akachukua baby wake mpya akaamua kumpeleka ili apate kitimoto, baby mpya akijua hapo walipokwenda jamaa hakuna namna anaweza kuwa keshawahi fika kwani dini yake hairuhusu.

Sasa walivyofika tu eneo la tukio, mpishi kwa bashasha kabisa akamkimbilia mteja wake wa siku zote na kumuuliza " Boss kama kawaida?"

Aisee kilichotokea hapo , ni kwa mpishi kukumbana na suluba ya aina yake toka kwa mteja wake mzoefu.

Tuwe makini na kauli hii, inaweza zua yasiyotabirika.
 
Ngoja nivute kiti niketi, nisubiri Michango ya WADAU kwa wingi
 
Ngoja nivute kiti niketi, nisubiri Michango ya WADAU kwa wingi

kuna sehemu nilikuwa nachukua kitimoto siku moja usiku nimeenda jikoni kuweka oda nikamuona jamaa kapiga kanzu anaweka ki hotpot ndani ya kanzu yani amenyanyua kanzu akaweka pale mbele ya tumbo afu akaamsha
 
kuna sehemu nilikuwa nachukua kitimoto siku moja usiku nimeenda jikoni kuweka oda nikamuona jamaa kapiga kanzu anaweka ki hotpot ndani ya kanzu yani amenyanyua kanzu akaweka pale mbele ya tumbo afu akaamsha
Kiongozi upo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…