Mshahara wa advanc bank kwa nafasi ya loan officer huwa ni bei gani?

Perry

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2011
Posts
10,058
Reaction score
2,195
Wakuu,naomba kwa anaejua mishahara ya hao jamaa huwa ni shiling ngapi,maana wameniita kwenye written interview kesho!
 
Sasa benki head office manzese unategemea nn?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Sasa benki head office manzese unategemea nn?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

ni kweli buku nane kwa siku halaf wateja unatafuta jua kali balaa matenti yao kama watu wa simu hawajali kama mtu una degree yako unalost pale u wont see urself growin in career wise unazungukuka madukani uswahilini yan unakuwa kama wauza mabesen na degree yako
 

Degree ni nini katika utafutaji wa maisha? Basi kama hiyo degree ni zaidi ya hiyo buku 8,nenda dukani mpe mangi hiyo degree alafu mwambie akupe unga robo na chenji irudi,acheni hizo mambo wadogo zangu,mwanzo ni mgumu sana.
 
Waambie aise, degree isikupe bichwa la kutaka kuanza na M2 ndo ujue sasa umeanza kazi, mwamzo mgumu watu wanasota na degree siku hizi hadi wanaamua kwenda kuongezea masters ndipo waingie sokoni.
 
Sasa benki head office manzese unategemea nn?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Cha kwanza mnachoweza kufanya mnapotoka vyuoni ni kuulizia mishahara na kukandia ofisi zilipo.

Labda nikukumbushe tu kuwa hata weledi wa huyu anayeomba kazi yenyewe haustahili kulipwa elfu 3 kwa siku. Kama umesoma kiasi cha kudhania unastahili kuomba kazi ya Loan Officer halafu una ukapuku kama wa kwake sidhani kama unastahili kulipwa zaidi ya 3,000 kwa siku.

Loan Officer ina maanisha atahusika na miamala ya fedha leo na kesho, lkn hata lugha ya fedha na manunuzi tu haijui. Angalia jinsi swali la kipuuzi kabisa lilivyochoropoka toka kwake: Mshahara wa advanc bank kwa nafasi ya loan officer ni bei gani?

Bei kwa bidhaa gani? Hiki ni kiswahili ambacho tumekiongea tangu utoto wetu, kesho hawa ndio wanatusainia mikataba bila kujua wameendika nini.
 
Hawa jamaa wakishatoka vyuoni wanakuwa na expectation kubwa sana! wanaota ndoto za ajabu sana. Yaani wanachojua ni kuwa watapata nafasi kubwa kubwa immediately na kulipwa mishahara minono then wanunue magari na kusihi kwenye nyumba kali, kama wako peponi vile!
Swali: Kwa kipi mlichonacho muanzie juu hivyo? au kwa kulishwa theories za mwaka 47? au kwa kwenda field kwa muda wa miezi mitatu ndo mmeshajua kazi?

Hivi mnajua soko la ajira lilivyo kwa sasa? vyuo vingapi vya ndani na nje vinamwaga graduates sokoni? je ninyi mpo competitive enough kuwashawishi waajiri wawape ajira bila kuingia gharama za training kwanza kuwapiga msasa? Lugha ya kibiashara je, Mnaijua? au ndo zile za kuungaunga na kudesa disertation?

Mnakandia ofisi ya Advans Bank kuwepo Manzese, kwa uelewa wenu wa kudesa hamjui hata target market ya hii bank. Jiulizeni kwanini access bank na advans bank zipo sehemu za watu wa kipato cha chini na kati kama vile manseze, mbagala etc na sio Masaki, Osterbay.

Graduates you must start thinking outside the box, our labor market is very saturated at the moment. Unatakiwa uwe flexible mwanzoni, pata ajira inayokupatia vijisenti kidogo huku ukiangalia alternatives.

Waambie aise, degree isikupe bichwa la kutaka kuanza na M2 ndo ujue sasa umeanza kazi, mwamzo mgumu watu wanasota na degree siku hizi hadi wanaamua kwenda kuongezea masters ndipo waingie sokoni.
 

No doubt utakuwa wa kike.

Bi mdogo, degree haimaanishi tiketi ya wewe kukaa ofisini. Degree ni kiwango cha elimu na sio kiwango cha UBOSI. He who works had is the boss. Upo uwezekano share holders wa Advans Bank ni mama lishe na makondakta wa daladala. What make them on top of you is their enthusiasm and entrepreneur mindset.

Huko walipo (share holders) wapo juani wakiuza mabeseni unayokandia ili waendelee kuwekeza zaidi katika uwekezaji ambao unakupa wewe ajira. Katika hali yeyote, usijidanganye kuwa wewe ni bosi kwao, WEWE NI MTUMISHI WAO.

Angalia hiyo kauli yako "hawajali kama mtu una degree yako". Hii ni kauli ya mtu masikini sana, tena fukara wa mawazo. Advans Bank hawakufungua firm yao ili wakuajiri. Yawezekana kutoa ajira ni moja ya sababu za kuanzishwa kwa institution lkn sidhani kama that was their primary objective. In business world the first thing on the line is MAKING PROFIT.

Sasa kwa kudhania kwamba ukiwa na degree maana yake huchomwi na jua huo (ashakhum si matusi) ni upumbavu. Kuna watu wana Masters (Geology, Civil Engineering, Marine Biology n.k) na wapo juani ili kutimiza majukumu yao. Au unadhani wewe ndio umesoma sana kuliko watu wote?
u wont see urself growin in career wise
Ukitaka kuandika paper yako juu ya tabia zinazoathiri SMEs Tanzania basi that is the right place. Hamia field. Hakuna namna Marine Biologist anaweza kufanya kazi bila kuwepo chini ya bahari hata awe na elimu gani. Na kama ulikuwa unataka kupatiwa kiyoyozi pale nje, basi fahamu kuwa kiyoyozi hakiji bila wewe na wenzako wenye degree (mliosoma sana) mtakapoamua kuweka juhudi zenu kuiinua Advans Bank ifikie level ya huko unakotaka kulinganishia. Unayoyaona CRDB, Standard Chartered na kwingineko hayakushuka na wala hayakuletwa na watu wenye mawazo kama yako, bali watu waliotambua thamani ya elimu zao inaonekana zinapozalisha kitu na sio kusujudia makaratasi.

Ukiendelea kuwaza unavyowaza, amini nakuambia utaishia kuhonga mwili wako kwa mameneja ktk harakati za kutafuta na hayo makaratasi yako yataishia kukupatia ugonjwa. Taifa hili halitajengwa kwa makaratasi bali kwa kufanya kazi kwa nguvu.

Reading from your JF ID (Wemah) ambayo bila shaka inasimama kwa Wema naweza kuona kuna shida kidogo ktk tafsiri ya maisha kichwani mwako. Ukiona Mushi (mchaga) anajiita Mushy, Msaki anajiita Msacky basi ujue kuna upungufu sehemu. Unaonekana ni mtu unayependa kuji - boost to ana extent jina lako mwenyewe WEMA, umeliongeza H just to sound English; Inferiority Complexion. Kama haitoshi, unakandia wauza mabeseni (for the way you speak) ilhali Business Chain inawahitaji wao zaidi yako (kama umesoma kweli utakubaliana na mimi katika hili)

NB: Karibu kwa ushauri ikiwa utautaka na nakaribisha matusi pia ikiwa kuna atakayejisikia kuwa annoyed na maneno yangu. Ila kwa tahadhari, kejeli na matusi ndio hasa fani yangu.
 
well said mkuu, wataokota japo kidogo. Siku wakifungua biashara zao afu wakapata changamoto za kukuza biashara then watakumbuka haya maandishi uliyoyaandika ku- expand think tank yao.

 

Ningeshangaa sana kama nisingekuta comment yako kwenye huu uzi......!!!
 
book 8 kwa siku kwa muda wa miezi mi3 ya kwanza !

Hapa kuna tatizo lamsingi kabisa...kuna hoja moja inayofanan na hii nilitofautiana sana na Mwana Mtoka Pabaya,lakini kwa kili naweza kumuunga mkono kwamba graduates mmeanza kupotoka!!!Labda nikuulize mtoa mada,wewe ulitegemea ukienda advans Bank utapewa kiasi gani kwa kufanya kazi ya loan officer????
 
Last edited by a moderator:
Da! pengine mimi ndio nina uelewa potofu juu ya ku'hold degree.
 
Wakuu safi sana kwa kuongea namimi naomba niongezee hapo kwanza kabisa napenda niseme kuwa hawa ma graduates wanakuwa na high expectations za kazi
Ila uwezo wao unakuwa hamna kitu wao wanajua kuwa kuwa na degree wakifika watakuwa na high salary gari zuri na kila kitu wamesahau kuwa pale ofisini kuna watu wana miaka tokea wananyonya na wana qualification zote

Degree au master ni kitu cha kawaida saana na sio kitu ambacho kitakufanya upate kazi ya maana ndio maana kuna kitu kinaitwa Experience experience ndio inayotakiwa je una experience ya miaka? Huna academic qualifications zenyewe ni za kuunga unga unategemea upate mkwanja wa ukweli

Pia ngoja niwaibie siri kwenye mabank hakuna pesa ni mentality tu ya watu nenda kwenye firm inayo consist masuala ya engeneering kama vile mining, fuels, electricity na kwenye NGO kubwa kubwa kama UN, Amref na Finca. Huko kwenye mabank hovyo tu unless upate bank ya kimataifa yenye branch tu hapa kama baclays, standard charterd, fbme, citi bank

Cha msingi na cha sekondary kukushauri ni kuwa ongeza masters dogo soko la ajira ni gumu kama unavyofikiri kuwa na master angalau unakuwa na something else ambayo itaku support tatu
Soma kozi mbali mbali ambayo unajua ita support kazi yako unayosomea itakusaidia
Ila uwe na maksi za kueleweka piga msuli usiwe kama wale wapumbavu wanaogoma kisa wanataka mikopo wanaacha kusoma kisa mikopo na wanashabikia kile chama cha magwanda wakiingia kwenye soko la ajira ni ushuzi mtupu
Nitarudi
 
Ningeshangaa sana kama nisingekuta comment yako kwenye huu uzi......!!!

Kama ulitegemea kunikuta kwenye mada za MMU naupa pole. ''Mke wa mtu anataka turudiane, wana JF je nikubali?''
''Shemeji yangu ananivalia khanga moja....nifanyeje wanaJF''

Naamini zipo ubaoni hizo mwende mkajadili. Mimi niache na vijana hapa wanahitaji msaada wangu
 

''By the time a man comes to realize that his father was right, he usually has a son who think he is wrong''


Si mbaya lakini mkuu, at last you came to your senses and understand the situation. Ile hoja haifanani na hii, this is much worse. Nina mashaka na uwezo wa wanaowafundisha, illusions!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…