Mshahara wa mfanyakazi huwa unapungua kila mwaka bila ya yeye mwenyewe kuelewa

Mshahara wa mfanyakazi huwa unapungua kila mwaka bila ya yeye mwenyewe kuelewa

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Mshahara wa mfanyakazi na wengine wenye kipato fixed kama wapokea pension huwa unapungua kila mwaka. Kinachokula mshahara wa watu hawa ni mfumuko wa bei. Kwenye mfumuko wa bei thamani ya pesa huwa inapungua.

Mfumuko wa bei wa 5% maana yake pesa imepungua nguvu kwa asilimia tano. Kama unapata mshahara wa 1m na mfumuko wa 5% ukatokea, basi hauna tofauti na mtu aliyepunguziwa mshahara kutoka 1m kuja 950,000 katika mazingira yasiyo na mfumuko.

Kama hujaongezewa mshahara kwa miaka mitano, na mfumuko wa miaka mitano ni 20%. Basi jua mshahara umeshushwa hadi 800,000.

Wanaopokea pensheni za kila mwezi ndiyo hatari zaidi sababu hakuna matumaini ya kuongezewa pensheni. Mfumuko unaweza kula pensheni na kukuacha masikini kila mwaka.

Hata ukiongezewa mshahara 3% na mfumuko ukawa 5%, jua kuwa mshahara umepungua kwa 2%.

Zamani wafanyakazi ndiyo walikuwa wenye maisha mazuri sana, siku hizi mfanyakazi hamkuti Chinga mwenye goli zuri kwa mapato. Chinga mapato yake yanaenda sambamba na inflation zinavyoenda. Mfanyakazi mshahara wake upo palepale au unaongezeka kidogo huku inflation inakimbia.

Serikali na waajiri wengine wanawezaje kulinda watumishi na wastaafu kutokana na inflation?
 
Mshahara wa mfanyakazi na wengine wenye kipato fixed kama wapokea pension huwa unapungua kila mwaka. Kinachokula mshahara wa watu hawa ni mfumuko wa bei. Kwenye mfumuko wa bei thamani ya pesa huwa inapungua.
izi mfanyakazi hamkuti Chinga mwenye goli zuri kwa mapato. Chinga mapato yake yanaenda sambamba na inflation zinavyoenda. Mfanyakazi mshahara wake upo palepale au unaongezeka kidogo huku inflation inakimbia.

Serikali na waajiri wengine wanawezaje kulinda watumishi na wastaafu kutokana na inflation?
Wangekiwa kwa value ya gold ama kwa dola. So wakitaka kukulipa wanacheki rate ya gold unalipwa labda hata unalipwa 0.34 ounce za gold. So wanacheki wanapiga hesabu wanapata dola ngapi wanabadilisha kwa your country money. Ukilipwa kwa stable currency or kwa gold nadhani Mambo Ni mswano
 
Wangekiwa kwa value ya gold ama kwa dola. So wakitaka kukulipa wanacheki rate ya gold unalipwa labda hata unalipwa 0.34 ounce za gold. So wanacheki wanapiga hesabu wanapata dola ngapi wanabadilisha kwa your country money. Ukilipwa kwa stable currency or kwa gold nadhani Mambo Ni mswano
Ingeweza kuwa nzuri kuliko sasa japo bei ya gold inakuwa manipulated sana na mataifa makubwa. Mfano wakitaka kununua huwa wanaishusha makusudi.
 
Mshahara wa mfanyakazi na wengine wenye kipato fixed kama wapokea pension huwa unapungua kila mwaka. Kinachokula mshahara wa watu hawa ni mfumuko wa bei. Kwenye mfumuko wa bei thamani ya pesa huwa inapungua.

Mfumuko wa bei wa 5% maana yake pesa imepungua nguvu kwa asilimia tano. Kama unapata mshahara wa 1m na mfumuko wa 5% ukatokea, basi hauna tofauti na mtu aliyepunguziwa mshahara kutoka 1m kuja 950,000 katika mazingira yasiyo na mfumuko.

Kama hujaongezewa mshahara kwa miaka mitano, na mfumuko wa miaka mitano ni 20%. Basi jua mshahara umeshushwa hadi 800,000.

Wanaopokea pensheni za kila mwezi ndiyo hatari zaidi sababu hakuna matumaini ya kuongezewa pensheni. Mfumuko unaweza kula pensheni na kukuacha masikini kila mwaka.

Hata ukiongezewa mshahara 3% na mfumuko ukawa 5%, jua kuwa mshahara umepungua kwa 2%.

Zamani wafanyakazi ndiyo walikuwa wenye maisha mazuri sana, siku hizi mfanyakazi hamkuti Chinga mwenye goli zuri kwa mapato. Chinga mapato yake yanaenda sambamba na inflation zinavyoenda. Mfanyakazi mshahara wake upo palepale au unaongezeka kidogo huku inflation inakimbia.

Serikali na waajiri wengine wanawezaje kulinda watumishi na wastaafu kutokana na inflation?
Uko sahihi kabisa mkuu!
 
Wangekiwa kwa value ya gold ama kwa dola. So wakitaka kukulipa wanacheki rate ya gold unalipwa labda hata unalipwa 0.34 ounce za gold. So wanacheki wanapiga hesabu wanapata dola ngapi wanabadilisha kwa your country money. Ukilipwa kwa stable currency or kwa gold nadhani Mambo Ni mswano
Idea nzuri sana hii... Hv mfano nkawa naajiriwa sehemu fulani naweza nikaamua wanilipe kwa Dollar?
 
Idea nzuri sana hii... Hv mfano nkawa naajiriwa sehemu fulani naweza nikaamua wanilipe kwa Dollar?
Hawawezi kukulipa Mana hawapo kwa ajili ya manufaa yako Bali Ni kwa ajili ya manufaa yao mkuu. Hii itakula kwao. Kuna shule moja Ada iko $$ so ukiweka tzs unacheki rate ya siku iyo ndio unalipa amount sawa na hizo dollars. Hapa mjanja unaweza subiria dola ikishuka value ndio unaenda kulipa Ada. Ni sawa na waziri anayeagiza magari from Japan ya wabunge anaagiza wakati yen ikiwa down so anasevu tzs kadhaaa.
 
Hapo ndipo utofauti kati ya ajira na kazi unaonekana
 
Back
Top Bottom