KERO Mshahara wa Waganga wafawidhi wa Zahanati na vituo vya Afya hauna tofauti na wa Daktari wa kawaida, Serikali itupatie posho ya madaraka

KERO Mshahara wa Waganga wafawidhi wa Zahanati na vituo vya Afya hauna tofauti na wa Daktari wa kawaida, Serikali itupatie posho ya madaraka

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Posho ya madaraka kwa waganga wafawidhi.

Kwa muda mrefu sasa, waganga wafawidhi wa zahanati na vituo vya afya nchini wamekuwa wakitekeleza majukumu mengi mazito ya kiuongozi bila kutambuliwa ipasavyo kwa malipo yao. Mbali na kuhudumia wagonjwa, sisi ndio tunasimamia watumishi, tunaratibu mipango kazi ya mwaka, tunasimamia ujenzi na miradi ya vituo, tunashughulikia mifumo ya hospitali, pharmacy, na kazi zote za clerking, pamoja na safari mbalimbali zinazohusiana na utendaji wa kituo.

Licha ya majukumu haya yote, mshahara wetu hauna tofauti na mganga wa kawaida ambaye jukumu lake kuu ni kuhudumia wagonjwa pekee. Hii ni hali isiyo ya haki na inaathiri morali ya wafanyakazi wa afya, hasa katika ngazi ya msingi ambako huduma za afya zinaanzia.

Tunaiomba Serikali na mamlaka husika zitambue mchango wetu na kutupatia stahiki yetu ya posho ya madaraka kama ambavyo inavyotolewa kwa viongozi wa sekta nyingine za umma.

Ni wakati wa kuwatendea haki wale wanaosimamia huduma za afya kwa bidii na uaminifu kwa manufaa ya wananchi wote.

#HakiKwaWagangaWafawidhi
 
POSHO YA MADARAKA KWA WAGANGA WAFAWIDHI.

Kwa muda mrefu sasa, waganga wafawidhi wa zahanati na vituo vya afya nchini wamekuwa wakitekeleza majukumu mengi mazito ya kiuongozi bila kutambuliwa ipasavyo kwa malipo yao. Mbali na kuhudumia wagonjwa, sisi ndio tunasimamia watumishi, tunaratibu mipango kazi ya mwaka, tunasimamia ujenzi na miradi ya vituo, tunashughulikia mifumo ya hospitali, pharmacy, na kazi zote za clerking, pamoja na safari mbalimbali zinazohusiana na utendaji wa kituo.

Licha ya majukumu haya yote, mshahara wetu hauna tofauti na mganga wa kawaida ambaye jukumu lake kuu ni kuhudumia wagonjwa pekee. Hii ni hali isiyo ya haki na inaathiri morali ya wafanyakazi wa afya, hasa katika ngazi ya msingi ambako huduma za afya zinaanzia.

Tunaiomba Serikali na mamlaka husika zitambue mchango wetu na kutupatia stahiki yetu ya posho ya madaraka kama ambavyo inavyotolewa kwa viongozi wa sekta nyingine za umma.

Ni wakati wa kuwatendea haki wale wanaosimamia huduma za afya kwa bidii na uaminifu kwa manufaa ya wananchi wote.

#HakiKwaWagangaWafawidhi

Kiongozi unahoja
waganga huko vijijini wanafanya kazi ngumu sana
Nakumbuka Dispensary yetu kule kijijini Nesi ana amshwa saa nane usiku kuzalisha au pengine kutibu mgonjwa hata sijui nani anamlipa. Nawaombea kwa Mungu awafanyie wepesi katika majukumu yenu
 
Kiongozi unahoja
waganga huko vijijini wanafanya kazi ngumu sana
Nakumbuka Dispensary yetu kule kijijini Nesi ana amshwa saa nane usiku kuzalisha au hata kutibu mgonjwa hata sijui nani anamlipa. Nawaombea kwa Mungu awafanyie wepesi katika majukumu yenu
Hapa umechanganya.

Mganga Mfawidhi hawezi kua dispensary.

Ila Mganga Mfawidhi ana jurisdiction hadi huko dispensary.

Ambaye yupo dispensary anakua ni incharge wa kituo. Huyu anaripoti kwa MOI (Mganga Mfawidhi) na DMO (District Medical Officer) ambaye ni mkuu wa idara ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe.
 
Mleta uzi naomba niulize kitu.

Naelewa MOI atakua na safari, pia anagewa pesa ya vocha zaidi ya 800K, anagewa nyumba, kwakua siyo mkuu wa idara hawezi kulipwa zile allowances za furniture and the like.

Kinachosababisha mshahara uwe sawa nafikiri ni kwakua MD yeyote akiwa na uzoefu serikalini wa angalau miaka 3 anatosha kua MOI. Ukiwa MOI hizo benefits nilizouliza hapo hazitoshi?
 
Mridhike na mishahara yenu.
Nikajua umasikini na mishahara midogo ni ya walimu tu kumbe SAGA linatembea chini kwa chini.

📌Hichi kilio mbona kama kina harufu na kusitishwa misaada ya MABEBERU.Why now???!!!!
 
Kiongozi unahoja
waganga huko vijijini wanafanya kazi ngumu sana
Nakumbuka Dispensary yetu kule kijijini Nesi ana amshwa saa nane usiku kuzalisha au pengine kutibu mgonjwa hata sijui nani anamlipa. Nawaombea kwa Mungu awafanyie wepesi katika majukumu yenu
eeh kaka mapambano wanayopitia wafanyakazi ni makubwa sana….. mzigo wa kazi ni mkubwa sana
 
Posho ya madaraka kwa waganga wafawidhi.

Kwa muda mrefu sasa, waganga wafawidhi wa zahanati na vituo vya afya nchini wamekuwa wakitekeleza majukumu mengi mazito ya kiuongozi bila kutambuliwa ipasavyo kwa malipo yao. Mbali na kuhudumia wagonjwa, sisi ndio tunasimamia watumishi, tunaratibu mipango kazi ya mwaka, tunasimamia ujenzi na miradi ya vituo, tunashughulikia mifumo ya hospitali, pharmacy, na kazi zote za clerking, pamoja na safari mbalimbali zinazohusiana na utendaji wa kituo.

Licha ya majukumu haya yote, mshahara wetu hauna tofauti na mganga wa kawaida ambaye jukumu lake kuu ni kuhudumia wagonjwa pekee. Hii ni hali isiyo ya haki na inaathiri morali ya wafanyakazi wa afya, hasa katika ngazi ya msingi ambako huduma za afya zinaanzia.

Tunaiomba Serikali na mamlaka husika zitambue mchango wetu na kutupatia stahiki yetu ya posho ya madaraka kama ambavyo inavyotolewa kwa viongozi wa sekta nyingine za umma.

Ni wakati wa kuwatendea haki wale wanaosimamia huduma za afya kwa bidii na uaminifu kwa manufaa ya wananchi wote.

#HakiKwaWagangaWafawidhi
 

Attachments

  • IMG_2448.jpeg
    IMG_2448.jpeg
    292.1 KB · Views: 3
  • IMG_2449.jpeg
    IMG_2449.jpeg
    283.1 KB · Views: 3
Back
Top Bottom