Mshambuliaji mpya wa Simba anatisha kweli shida yangu amesharogwa kabla hajaingia dimbani, tusipomtengeneza tutamtukana mara moja

Leonel Ateba Mbinda

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2023
Posts
644
Reaction score
2,695
Jamaa analijua goli sio masihara, anafunga mabao katika mazingira magumu sana huyu Mgambia, ana nguvu, mrefu ana mashuti na kasi ya ngiri, shida yangu ni kuwa kwa vile timu yetu imekosa kitengo kizuri cha superstition basi tutarajie striker huyu kuonekana mchovu.

Watu washampigia hesabu tayari wammalize vipi, wamepanga kutumia njia ile ile waliyotumia kummaliza Baleke ambaye hakika sasa hivi goli halioni tena, nawashauri viongozi wa mnyama striker wetu mpya asiingie kizembe nchini, mrudisheni kwao kwanza akaweke mazingira vizuri kwa sababu Gambia wenyewe mambo haya ya superstitions wako vzr mno, msipofanya hivi striker huyu anakwenda kuchekesha.

Mchezo mbaya sana umefanyika kwa wachezaji wetu ndio maana timu yetu imekuwa nyepesi sana, na tusipoangalia wale wajinga waliotufunga mabao 5 wanaweza kutupiga tena.
 
Angekuwa mchezaji mzuri asingekuwa na rekodi ya kuachwa Kila anapoenda au kutolewa kwa mkopo, pia asingekaa bila timu kwa miezi 8 ilo ni garasa lingine mmeleta usianze kutafuta kichaka Cha kujifichia hapa eti amesharogwa🤔🤔
Amerogwa au mmebeba takataka nyingine!
 
Kavideo akifunga magoli katika mazingira magumu tafadhali. Mbali na hapo simba mnajifariji tu na mkicheza mtakandwa na kulliwa kama mlandege anavyojipigia ndege zake
 
Baleke kajiendea zake mazembe
 
Acha Imani za kishirikina
 
Bocco ndio anawaumiza wenzake pale simba bila kuondoka hakuna striker atadumu simba yule jamaa ni hatari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…