Mshtakiwa akana kumtambua Sabaya

Mshtakiwa akana kumtambua Sabaya

mshale21

JF-Expert Member
Joined
Apr 8, 2021
Posts
2,126
Reaction score
5,068
Arusha.

Mshitakiwa wa tatu katika kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, Daniel Laurent Mbura (31), ameieleza mahakama kuwa hamtambui mshitakiwa wa kwanza wala wa pili katika shauri hilo na alifahamiana nao walipofikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Juni 4.

Akijitetea mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Odira Amworo shahidi huyo pia amekanusha majina yaliyopo kwenye hati ya mashitaka ambayo yanasomeka kama Daniel Gabriel Mbura wakati yeye jina lake ni Daniel Laurent Mbura.

Shahidi huyo aliiomba mahakama kupokea vyeti vyake viwili kuthibitisha majina yake na mahakama ikavipokea.

Akiongozwa kutoa ushahidi wake na Wakili anayemtetea, Fridolin Gwemelo, mshitakiwa wa tatu katika shauri hilo alisema Februari 9 alikuwa nyumbani na hakutoka siku nzima.

sabayapic-data.jpg
Chanzo;Mwananchi
 
[emoji91][emoji91][emoji91]
Hapa me bado najiuliza, huyu ndug hapo awali alitaja jina la Kati feki ili aje akane kuwa sio yeye!!? Au Hilo jina alielitaja wakati wa kuchukua details za mtuhumiwa Ni nani?

#ngoja tufuatilie hukumu itakuwaje
 
Waache wajifanye hawajuani tu ila kitaeleweka mwisho wa siku.

Kwa miezi kibao mnazurura wote leo mjifanye hamjuani kwani mlikuwa mnatembea gizzani si mapicha kibao yanawaonesha mkiwa pamoja
 
Hakuna kesi hapo bwashee.

Kila siku majina yanakosewa.
Umeshawahi kusikiliza hata kesi moja ya ngazi ya mwenyekiti wa mtaa?

Ukikuwa na ukawa na nyumba yako,utaitwa mtaani kwako isikilizwe hata shauli moja la ugomvi wa mke na mume ,ndipo utajua maana ya kesi.
 
Hiyo kesi ilitengenezwa na Mbowe kwa lengo la kulipa kisasi kwa Sabaya baada ya kukosa ubunge
 
Back
Top Bottom