Mshtakiwa kesi ya kusafirisha walemavu, kuwatumia kuomba afariki dunia

Mshtakiwa kesi ya kusafirisha walemavu, kuwatumia kuomba afariki dunia

GeoMex

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2014
Posts
5,431
Reaction score
19,913
Screenshot_20210209-155130_1612875130058.jpg

Dar Es Salaam. Mshatakiwa wa kwanza katika kesi ya kufanya biashara haramu ya kusafirisha binadamu, kukwepa kodi na kuisababishia hasara ya Sh31milioni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Sadikiely Meta(71) amefariki dunia katika Hospitali ya Temeke alikokuwa akipatiwa matibabu.

Meta na wenzake 14 wanakabiliwa na kesi uhujumu uchumi namba 2/2021 yenye mashtaka 41 yakiwemo ya kusafirisha na kutumikisha walemavu katika biashara ya kuomba barabarani inayosikilizwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu.

Robert Langeni ambaye ni wakili wa Meta ameeleza hayo mahakamani leo Jumanne Februari 9, 2020 mbele ya hakimu mkazi mkuu, Kassian Matembele wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa.

Langeni amesema Meta aliugua akiwa gerezani na kupelekwa katika hospitali ya Temeke kwa matibabu lakini Januari 28, 2021 alifariki dunia.

"Meta alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na tayari mazishi yamefanyika wiki iliyopita huko Moshi mkoani Kilimanjaro," amesema Langeni.

Awali, wakili wa Serikali, Kija Luzungana ameieleza mahakama hiyo kuwa kesi hiyo iliitwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haujakamilika.
Hakimu Matembele baada ya kusikiliza hoja za pande zote aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 23, 2020 itakapo tajwa.

Kesi hiyo imeendeshwa kwa njia ya video, huku washtakiwa14, wakiwa gerezani kutokana na mashtaka yanayowakabili likiwemo la kutakatisha fedha kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.

Mbali na Meta washtakiwa wengine ni Yusuph Mbuani (35), Joseph Magafu (20), Emmanuel Salu, Gogad Mayenga(18), Samson Akunahai (26), Husein John(18).

Wengine ni Zacharias Paul( 18) Dotto Shigula(19), Petro Simon(21), Emmanuel Sahani(38), Joseph Mathias (20), Massanja Paul (21), Aminiel Sangu (21) na Emmanuel Lusinge(25) maarufu Salimu.


Chanzo: Mwananchi
 
Kila siku imekuwa ni habari za vifo.

Kuumaliza mwaka huu kwa hakika itakuwa ni sawa kabisa na jina la ubini wake waziri mkuu wetu mpendwa bwana Kassim.
 
Kila sikuwa imekuwa ni habari za vifo.

Kuumaliza mwaka huu kwa hakika itakuwa ni sawa kabisa na jina la ubini wake waziri mkuu wetu mpendwa bwana Kassim.
Hakika ni majaliwa yake Mungu kuuona mwaka! R.I.P Sadikiely Meta
 
Kila sikuwa imekuwa ni habari za vifo.

Kuumaliza mwaka huu kwa hakika itakuwa ni sawa kabisa na jina la ubini wake waziri mkuu wetu mpendwa bwana Kassim.
kwani zamani watu walikuwa hawafi au ulikuwa husikilizi kipindi cha matangazo ya vifo redio one
 
kwani zamani watu walikuwa hawafi au ulikuwa husikilizi kipindi cha matangazo ya vifo redio one

Ni ukweli kuwa zamani watu walikuwa hawafi kwa corona jombi!

Hii ya kujitoa ufahamu kuhalalisha vifo kizezeta zezeta hivi mbona ilishaongelewa sana. Wala huna jipya. Machampioni wa ngonjera hizo walishaziacha kwa maana hazilipi:


Uliwahi kujiuliza nia ya kutokufanya postmortem au autopsy kwenye mfululizo wa vifo vifo hivi ili baadaye kusema hata zamani watu walikuwa hawafi ni nini?

Fumbo wafumbieni wajinga:

 
Maskini mzee Meta du Jiwe ndio kaishakosa hela zake za faini kwa makosa pendwa aliyopewa uhujumu uchumi na utakatishaji fedha , malengo ya ukusanyaji mapato ya DPP yamefeli .
 
Back
Top Bottom