blackberry m
JF-Expert Member
- Apr 16, 2012
- 563
- 414
Habari za jioni wakuu…
Poleni na majukumu ya kulijenga taifa na kujitafutia chochote kile ili mkono uende kinywani.
Nia na dhumuni langu kuandika waraka huu, ni kupata usaidizi/ushauri na hata utatuzi/tiba ya tatizo linalonisumbua. Tatizo langu naweza kuliita la pekee (najua ninalo peke yangu), kwani sijawahi sikia au soma mtu akiwa ameandika humu ukiachilia mbali kusimulia.
Tatizo ni kwamba, kabla ya kulala au kuchukuliwa na usingizi ni lazima nipate mshtuko kidogo ndipo niweze kulala. Ni muda sasa kwani nakumbuka kuwa nilikuwa nalo tangia zama zangu za utoto hata sasa.
Nakumbuka nyakati za utoto nilikuwa nahisi kama naruka kwenye mti (kudondoka), kisha nikishtuka na kulala tena hiyo njozi haijirudii tena hadi ifike siku nyingine.
Sasa nyakati hizi njozi hizo hakuna ila najikuta nashtuka tu na kisha kufuatiwa na usingizi mzito. Yeyote mwenye kufahamu na kujua tiba rasmi ya tatizo langu, tafadhali asisite kunieleza.
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu…
Poleni na majukumu ya kulijenga taifa na kujitafutia chochote kile ili mkono uende kinywani.
Nia na dhumuni langu kuandika waraka huu, ni kupata usaidizi/ushauri na hata utatuzi/tiba ya tatizo linalonisumbua. Tatizo langu naweza kuliita la pekee (najua ninalo peke yangu), kwani sijawahi sikia au soma mtu akiwa ameandika humu ukiachilia mbali kusimulia.
Tatizo ni kwamba, kabla ya kulala au kuchukuliwa na usingizi ni lazima nipate mshtuko kidogo ndipo niweze kulala. Ni muda sasa kwani nakumbuka kuwa nilikuwa nalo tangia zama zangu za utoto hata sasa.
Nakumbuka nyakati za utoto nilikuwa nahisi kama naruka kwenye mti (kudondoka), kisha nikishtuka na kulala tena hiyo njozi haijirudii tena hadi ifike siku nyingine.
Sasa nyakati hizi njozi hizo hakuna ila najikuta nashtuka tu na kisha kufuatiwa na usingizi mzito. Yeyote mwenye kufahamu na kujua tiba rasmi ya tatizo langu, tafadhali asisite kunieleza.
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwenu…