Msiba wa sheikh nassor bachu

Akthoo

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2007
Posts
1,001
Reaction score
1,021
innalillah wainna illahi rajiun.
Hatimae leo sheikh wetu , kipenzi cha waumini afrika mashariki amerejea kwa kwa mola wake. Mwenyezi mungu amuwie radhi.
Tunamwomba allah, awape nguvu na subira familia yake na waumini wote kustahamili msiba huu mkubwa.
 
Thread yako ina mapungufu makubwa sana, kwahiyo wasiowaumini hili tangazo haliwahusu? halafu huyu ni allah au Allah?

Msiba huu ni mkubwa je kuna msiba mdogo? hivi na Mashekh siku hizi ni Ma-celeb? jipange kabla ya kuandika thread humu.
 
watu wengine wanaleta uzi za kichokozi!! sasa hayo maneno "innalillah wainna illahi rajiun". si utafsiri kwa kiswahili? ndio nyie mnaleta udini humu ndani.
 
watu wengine wanaleta uzi za kichokozi!! sasa hayo maneno "innalillah wainna illahi rajiun". si utafsiri kwa kiswahili? ndio nyie mnaleta udini humu ndani.

sasa hapo kamchokoza nani?.kama uliona haikuhusu ungeenda thread nyingine,au walitafuta beef we mama eh?
 
Sheikh Nassor Bachu ndio alkuwa sheikh wa wapi?
Ungeimdadavua vizuri tupate kumjua
 


Hapo kwenye bluu inaonyesha wewe ni mbaguzi na mdini mkubwa.....msiba ni kwa jamii nzima acha udini wako wewe!!!!!!!!

innalillah wainna illahi rajiun
 
Thread yako ina mapungufu makubwa sana, kwahiyo wasiowaumini hili tangazo haliwahusu? halafu huyu ni allah au Allah?

Msiba huu ni mkubwa je kuna msiba mdogo? hivi na Mashekh siku hizi ni Ma-celeb? jipange kabla ya kuandika thread humu.


Sawa; Nitajipanga! Tunajifunza kutokana na makosa. Kuhusu matumizi ya "Capital/ small letters" ni ujuzi wa ku "set" umenibabaisha. Ukweli nimeandika kutumia "capital letters" pekee lakini nilipo "post" maandishi yametokea hivi.
Naam; kuna misiba midogo na mikubwa bila shaka. Mfano Msiba wa Mwalimu Nyerere utaulinganisha na Sharobaro?

Na msiba unawagusa na kuwaumiza zaidi wale wanaokuwa karibu na marehemu.
 
naona chuki ya waziwazi juu U-Islam, sijaona dalili ya udini katika post lakini mtu ameitwa mdini duh, sidhani kama kuna anayelazimishwa kuchangia thread, kama hujaelewa lugha acha walioelewa wachangie kwani wewe siyo muhimu sana.
 
Thread yako ina mapungufu makubwa sana, kwahiyo wasiowaumini hili tangazo haliwahusu? halafu huyu ni allah au Allah?

Msiba huu ni mkubwa je kuna msiba mdogo? hivi na Mashekh siku hizi ni Ma-celeb? jipange kabla ya kuandika thread humu.

ipo tofauti ya msiba mkubwa na mdogo, mhusika aliyefikwa na msiba kwake ni msiba mkubwa ila kwa watu baki ni msiba mdogo kwao wao. According to the thread, msiba ni mkubwa kwa Waumini wa ki-Islam, ila ni mdogo kwenu msioonyesha kujali na kushupalia kumkosoa mwandishi.
 
Wagalatia waombeni mods wawatoe waislamu wote humu ili mtumie kutangaza misiba ya mitume na manabii wenu na mambo ya kanisa tu maana hizo chuki sasa zimezidi
 
Kwan huyo sheikh ni wa wapi??yaan ungeweka hata utangulizi kidogo.Kuna mtu alipost msiba wa askofu mmoja wa kanda ya kaskazini,alianza na utangulizi,hata kwa mtu ambaye hamfaham anaweza kupata picha....ila kwa hii naona uliteleza mkuu....NO RIP(simfahamu)
 
sasa hivi sala ya maiti ndio anaswaliwa al marhum sheikh nassor bachu katika viwanja vya mnazi mmoja , zanzibar
 
naona chuki ya waziwazi juu U-Islam, sijaona dalili ya udini katika post lakini mtu ameitwa mdini duh, sidhani kama kuna anayelazimishwa kuchangia thread, kama hujaelewa lugha acha walioelewa wachangie kwani wewe siyo muhimu sana.

Kuna watu wakiwemo lazima waharibu tu. Hujambo Matola ?, nimekumiss
 
Last edited by a moderator:
Angekuwa Askofu Fulani wasingeuliza jukwaa wala nini..ndio maana siyapendi haya matoto ya CHADEMA!
 
Siku nikisikia mwanangu kajiunga na hawa wahuni...
 
Thread yako ina mapungufu makubwa sana, kwahiyo wasiowaumini hili tangazo haliwahusu? halafu huyu ni allah au Allah?

Msiba huu ni mkubwa je kuna msiba mdogo? hivi na Mashekh siku hizi ni Ma-celeb? jipange kabla ya kuandika thread humu.
kutokana na mgogoro ulioibuka hapa donge kwenye mazishi ya sheikh nassor bachuu pale kaburi lake lilipochimbwa karibu na msikiti kitu ambacho kwa mujibu wa ahli sunna ni kosa na wamekataa kabisa kumzika hapo na tayari wamekaa kikao pamoja na wanafamilia na wameshatoa uamuzi kupitia sheikh nurdin kishki na kinachofuata hivi sasa ni kuchimbwa kaburi jengine na wamewataka maelfu ya waislamu waliofika hapo kuwa na subra HII NI NOW NOW
 

Pole, wala hahitaji RIP yako.
 
sasa hivi sala ya maiti ndio anaswaliwa al marhum sheikh nassor bachu katika viwanja vya mnazi mmoja , zanzibar
na mgogoro umeiibuka hapa donge kwenye mazishi ya sheikh nassor bachuu pale kaburi lake lilipochimbwa karibu na msikiti kitu ambacho kwa mujibu wa ahli sunna ni kosa na wamekataa kabisa kumzika hapo na tayari wamekaa kikao pamoja na wanafamilia na wameshatoa uamuzi kupitia sheikh nurdin kishki na kinachofuata hivi sasa ni kuchimbwa kaburi jengine na wamewataka maelfu ya waislamu waliofika hapo kuwa na subra
 
Smile kuna Mpemba kaiba password yako ndio anapost humu siamini kama huyu ni wewe, kuna code number humu za kuwagunduwa Mujahidina miandiko yao naijuwa vyema.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…