Msimamo wa wanasheria kuhusu law school

ba nso

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2012
Posts
668
Reaction score
225
Naomba maoni yenu wadau. Hivi ni sawa kusema mhitimu wa sheria hapaswi kuajiliwa mpaka aende law school? Mimi binafsi si muumini wa hii kitu na sioni sababu za msingi kuthamimisha Llb ya miaka 3au 4 kwa kozi ya miezi 9. Maoni tafadhal
 
Naomba maoni yenu wadau. Hivi ni sawa kusema mhitimu wa sheria hapaswi kuajiliwa mpaka aende law school? Mimi binafsi si muumini wa hii kitu na sioni sababu za msingi kuthamimisha Llb ya miaka 3au 4 kwa kozi ya miezi 9. Maoni tafadhal

Kuna mahala imeandikwa kuwa mhitimu wa sheria hapaswi kuajiriwa?
 
Kuna mahala imeandikwa kuwa mhitimu wa sheria hapaswi kuajiriwa?

unaijua the law school o tanzania act? Hiyo sheria ndo inavosema isome utaona my concern . Na waajiri wanataka wahitimu wa law school
 
unaijua the law school o tanzania act? Hiyo sheria ndo inavosema isome utaona my concern . Na waajiri wanataka wahitimu wa law school

Kwa hiyo ina maana ukisomea sheria basi wewe huwezi kabisa kufanya kazi ingine yoyote ile hadi uwe umepitia hayo mafunzio ya law school?

Yaani hata hata umeneja wa duka hupaswi kufanya/kuwa?

That's stupid.

Tafadhali hebu iweke hiyo law school act hapa.
 
Nenda law school acha uoga au ulipata supp ndo maana unaona law school haina umuhimu? Dhumuni la shule ya sheria Tanzania ni kutoa mafunzo ya sheria kwa vitendo na sio nadharia kama inavyotolewa vyuoni. Ukisoma 'the Law School of Tanzania Act, 2007' utaona inasema mtu asiajiriwe kazi za kisheria kama hajapita shule ya sheria. In practice kati ya 2009 hadi sasa waajiriwa wa mahakamani ie mahakimu na wasaidizi wa mahakama sio lazima wawe wamepita law school. Ila kazi nyingine za kisheria bado wanahitaji upitie law school of Tanzania. Pia ili uwe wakili ni lazima upite na kufaulu law school, hii ni kwa wale waliomaliza baada ya 2007. Kama unaona sheria kuna complications hukatazwi kufanya kazi nyingine kama kuwa bank teller, kufanya kazi madukani nk,
 
Law School haikwepeki kwa anayehitaji kuwa Wakili. Kama huitaji kuwa Wakili,si lazima uende Law School.
 
Law school ni muhimu katika kuwanoa wahitimu wa sheria. Kimsingi LS ni sehemu ya kufanyia vitendo yale yote uliyopata kwa nadharia. Kwa mfano, kwenye theory mnafundishwa kitu kama Mens rea katika Criminal Law. Mwanasheria anajua kuwa hii ni mental element of the offence. Ukienda kwenye LS utaweza kujua dhana hii inavyofanya kazi na kupitia vitendo unaweza kui-establish pasina kudhani kama kwenye nadharia. Ni Tanzania tu iliyochelewa kuwa LS. Nchi nyingi hata za kiafrika bila kwenda LS hujawa mwanasheria kivitendo bali kinadharia.
 
Hivi kwa nini kuwe na tofauti kati ya law school na UDSM kitivo cha sheria?

Mbona kwa wenzetu ukitoka law school unakuwa kamili gado na kinachobaki ni kufanya bar exam tu kama unataka kuwa wakili. Sasa kwa nini Tanzania iwe tofauti hivyo?

Kwa wenzetu ukienda law school maana yake ni kwamba unaenda kujifunza yote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…