Msimlaumu sana Mwigulu, pengine anafuata tu maelekezo

Msimlaumu sana Mwigulu, pengine anafuata tu maelekezo

Parody

Member
Joined
Sep 13, 2020
Posts
24
Reaction score
69
Wakuu, nawasalimu kwa Jina la Jamhuri.

Nimepita mitandaoni, nimeona jinsi watu wanavyomshambulia Mwigulu kuhusu tozo ya miamala. Naunga mkono mashambulizi, lakini nadhani tunakosea tunayemwelekezea mashambulizi hayo.

Wanasema kila zama na kitabu chake. Wakati wa enzi za Mwendazake, taifa lilikuwa na ajenda ya kuondoa hofu kuhusu corona, na moja kati ya njia zilizotumika ni kuhakikisha ugonjwa wa corona unaonekana si lolote, na kuwa umeletwa na mabeberu, na kuwa hii ni vita ya kiuchumi.

Sasa, ili kufanikisha ajenda hiyo, ilibidi apatikane mtu atakayeongoza mapigano kwa niaba ya Mwendazake. Chaguo la kwanza lilikuwa Dkt. Ndugulile kwa kuwa alikuwa Waziri wa Afya. Kwa jinsi ninavyomfahamu, Dkt Ndugulile ni daktari kwa taaluma, na anawajibishwa na kiapo chetu cha Hippocratic Oath. Asingeweza kuupotosha umma kwa maslahi ya kisiasa. Na hicho ndicho alichokifanya. Kwa kuwa alionekana hawezi kutekeleza maagizo, ikabidi apaki pembeni.

Akaletwa mama yetu. Picha la kwanza, kaanza na scarf za bendera ya Tanzania (Naanza kuwa na wasiwasi na hawa wanaovaa scarf na tai za bendera maana Mwigulu naye humohumo 😁). Maelezo yasiwe mengi, tunajua alichokifanya. Sasa zama za Mwendazake zimepita na kitabu chake (ingawa bado tunaendelea kuisoma namba kwenye kitabu hicho). Zimekuja zama za Kazi Iendelee.

Mtazamo wangu ni kuwa ajenda ya zama hizi kwa sasa ni kuhakikisha mjadala wa katiba mpya unazimwa kwa nguvu zote, na ili kufanikisha ajenda hiyo, lazima litafutwe jambo zito litakalowaondoa Watanzania kwenye kujadili katiba mpya. Jambo lenyewe ni Kodi ya kipumbavu inayomgusa mwananchi moja kwa moja.

Mnakumbuka hadithi ya Sungura na jogoo wa baba? Jinsi sungura alivyofanikiwa kumtupia mbwa mifupa ya jogoo ili apate mwanya wa kutoroka? Ndicho kinachofanyika sasa. Mwigulu anatumika tu kama scapegoat na anafuata tu maelekezo. Suala la tozo ya miamala ni kubwa kuliko Mwigulu, na kumkaanga Mwigulu ni kuharibu mafuta kwa mtu asiyestahili. Mkaangeni anayempa maelekezo Mwigulu.

Nawasilisha kwenu Wakuu, naomba mjadala uwe wa staha.
 
Mnyalu Mgimwa aligoma kufuata maelekezo alijikita kwenye ubobezi wa taaluma ya fedha!
 
Mkuu kama kuna watu ambao hawampendi mama nahisi mi ni namba 1 lakini kwenye hii tozo najikuta tu nahisi ni sahihi sema ina mapungufu kidogo

1)muamala mmoja kukatwa mara 2
2)mlipa kodi halali tena bado analipa na kodi nyingine

Mama angeweka tozo za makundi
Mfano;wangetathimini wale wanaolipa kodi wangeombwa kupeleka namba ya simu 1 ambayo angekuwa anatuma au kutoa pesa bila tozo hapa kungekuwa na kundi la waajiriwa na wafanyabiashara ambao leseni zao ni hai ndo wangekuwa na msamaha huo na pindi leseni inapoisha muda unaingia kwenye tozo siku hiyo

Nahisi kama ingesaidia kuweka usawa wa kodi ila sijajua pia kama kungekuwa na changamoto gani?

Ila wazee tulipe tu kodi najisikiaga vibaya maraisi wanapoomba msaada hadi kwa vinchi tunavyovizidi rasilimali watu
 
Ni kweli Mwigulu hana ubavu juu ya suala hili isipokuwa anafuata maelekezo ya bosi wake tu na bosi wake ametuangusha sana hadi tumeanza kuwaza kuwa huenda si mwenzetu kwa sababu:
1,2,3,4,5,.....
 
Mimi namlaumu Mwigulu huu ubogus unatoka kwake.

Nilikuwa namkubali sana Nalaila Kiula miongoni mwa Wanyiramba.
 
Mimi namlaumu Mwigulu huu ubogus unatoka kwake.

Nilikuwa namkubali sana Nalaila Kiula miongoni mwa Wanyiramba.
Napata wakati mgumu kuamini kuwa Mwigulu ndie Mastermind wa hii kodi. Sawa, ameshiriki kuota moto wa wajinga na sasa ni zamu yake kuteka kuni, anatumika tu
 
Mkuu kama kuna watu ambao hawampendi mama nahisi mi ni namba 1 lakini kwenye hii tozo najikuta tu nahisi ni sahihi sema ina mapungufu kidogo

1)muamala mmoja kukatwa mara 2
2)mlipa kodi halali tena bado analipa na kodi nyingine

Mama angeweka tozo za makundi
Mfano;wangetathimini wale wanaolipa kodi wangeombwa kupeleka namba ya simu 1 ambayo angekuwa anatuma au kutoa pesa bila tozo hapa kungekuwa na kundi la waajiriwa na wafanyabiashara ambao leseni zao ni hai ndo wangekuwa na msamaha huo na pindi leseni inapoisha muda unaingia kwenye tozo siku hiyo

Nahisi kama ingesaidia kuweka usawa wa kodi ila sijajua pia kama kungekuwa na changamoto gani?

Ila wazee tulipe tu kodi najisikiaga vibaya maraisi wanapoomba msaada hadi kwa vinchi tunavyovizidi rasilimali watu
Naunga mkono Mkuu.. hizi tozo zinahitaji marekebisho makubwa kama kweli tuna nia ya dhati ya kuisaidia nchi yetu.. Kama vipi zifutwe tu serikali ina njia nyingi za kukusanya mapato bila kuwaumiza wananchi wa kipato cha chini
 
Back
Top Bottom