Mwamuzi wa Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 15,486
- 45,256
Habari!
Nilitaka kuandika kitabu muda kidogo chenye title inayosema "Kanisa la uzinzi" ila nimekosa muda kidogo, ila ipo siku nitaandika hichi kitabu ili angalau watu wachache wapone.
Kanisa la sasa limepatikana, silaha ya mwisho ya Ibilisi ambayo ni roho ya uzinzi inafanya kazi kwa kasi sana.
Uzinzi hauangalii jinsi unavyonena kwa lugha au jinsi unavyotoa pepo wachafu kwa watu wengine.
Uzinzi una njia mbili tu za kuukwepa.
1. Kuukimbia
2. Kukataa (kuukemea)
Hii njia namba 2 inaanza kwa kiongozi kisha muumini binafsi aukatae na kuukemea.
Wachungaji hawana ujasiri wa kukemea uzinzi kwakuwa nao wana vifungo vya uzinzi.
Ukimwona mchungaji wako anahubiri mara 5 na hagusii hili janga la uzinzi jua tu naye yuko kifungoni na hajui anatokaje.
Zamani ukizini tu lazima mzee wa kanisa au mchungaji atajua na atakuita akuambie asemayo Mungu ila sasa kanisa liko na giza totolo, halioni tena.
Labda sadaka tu ndizo zinaonekana kwa macho ya rohoni na mwilini maana ndio msingi mkubwa wa makanisa ya sasa .
Nilitaka kuandika kitabu muda kidogo chenye title inayosema "Kanisa la uzinzi" ila nimekosa muda kidogo, ila ipo siku nitaandika hichi kitabu ili angalau watu wachache wapone.
Kanisa la sasa limepatikana, silaha ya mwisho ya Ibilisi ambayo ni roho ya uzinzi inafanya kazi kwa kasi sana.
Uzinzi hauangalii jinsi unavyonena kwa lugha au jinsi unavyotoa pepo wachafu kwa watu wengine.
Uzinzi una njia mbili tu za kuukwepa.
1. Kuukimbia
2. Kukataa (kuukemea)
Hii njia namba 2 inaanza kwa kiongozi kisha muumini binafsi aukatae na kuukemea.
Wachungaji hawana ujasiri wa kukemea uzinzi kwakuwa nao wana vifungo vya uzinzi.
Ukimwona mchungaji wako anahubiri mara 5 na hagusii hili janga la uzinzi jua tu naye yuko kifungoni na hajui anatokaje.
Zamani ukizini tu lazima mzee wa kanisa au mchungaji atajua na atakuita akuambie asemayo Mungu ila sasa kanisa liko na giza totolo, halioni tena.
Labda sadaka tu ndizo zinaonekana kwa macho ya rohoni na mwilini maana ndio msingi mkubwa wa makanisa ya sasa .