Msingi wa UNGA ni muhimu kwa uhusiano wa pande nyingi

Msingi wa UNGA ni muhimu kwa uhusiano wa pande nyingi

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
VCG41N537851711 (1).jpg


Hivi karibuni, Rais wa Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa (UNGA) Csaba Korosi alifanya ziara ya siku nne nchini China, ambapo alikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa ngazi ya juu wa serikali ya China.

UNGA ni chombo kikubwa cha majadiliano cha Umoja wa Mataifa, na ni jukwaa muhimu kwa utungaji wa sera za dunia, na kinapaswa kuongoza kwa mamlaka kikiwa na lengo la kukabiliana na masuala ya dunia kupitia maafikiano, umoja na ujumuishi.

Ujumbe wa ziara ya Korosi China ni wa wazi, kwamba ni muhimu kulinda uhalisia kamili wa pande nyingi wa kutegemeana kwa maendeleo ya binadamu na usalama wa kimataifa.

Katika dunia yenye mmomonyoko wa taasisi za kitaifa na kimataifa, majadiliano yanayozungumzia kwa upana masuala ya kimataifa yaliyoorodheshwa kwenye Mkataba wa Umoja wa Mataifa yanapaswa kuendelea bila kupingwa.

Alipokutana na Bw. Korosi, Waziri wa Mambo ya Nje wa China Qin Gang alisema UNGA ni chombo cha juu zaidi cha wote na cha uwakilishi cha Umoja wa Mataifa. Amesema kudumisha mfumo wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa kupitia utaratibu wa dunia uliojikita katika sheria ya kimataifa, kama China inavyofanya, pia ni jambo la muhimu sana.

Kwa mfano, kutimiza kwa kasi kwa malengo 17 ya Ajenda ya Maendeleo Endelevu kunaweza kufikiwa endapo nafasi ya UNGA haitatekwa na hatua za upande mmoja za nchi wanachama. Zaidi, utekelezaji wa kasi wa mapendekezo mengine kama Pendekezo la China la Maendeleo ya Dunia (GDI) ambalo linatokana na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Mwaka 2030 ya kujenga maendeleo ya dunia ambayo ni imara, ya kijani na yenye afya, utawezesha malengo ambayo yananufaisha jamii nzima ya kimataifa, na hili linawezekana kama moyo wa uhusiano wa pande nyingi utafuatwa.

Pia, jamii ya kimataifa inapaswa kujitahidi kuhakikisha kuwa rasilimali zinazopatikana kwa taasisi za Umoja wa Mataifa zinatumika kwa ajili ya uwezeshaji wa sera zinazolenga kudumisha amani na kuboresha maendeleo. Mfano mzuri ni haja ya kuendeleza uwekezaji katika mwaka 2023 kwa ajili ya taasisi za Umoja wa Mataifa kama vile Sekretarieti ya Umoja huo, ambayo inaweka ajenda za majadiliano na taasisi za maamuzi za Umoja wa Mataifa kama vile Baraza Kuu la Umoja huo.

Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zinaweza kutoa mchango chanya katika kuimarisha mifumo inayopambana na changamoto zilizopo sasa duniani. Katika mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje wa China Qin Gang, Bw. Korosi alisema Umoja wa Mataifa unaweka umuhimu mkubwa katika ushawishi wa China na nafasi yake ya uongozi katika kuboresha utawala, kuanzisha majadiliano kati ya nchi ili kumaliza tofauti zao na kuboresha umoja kwa ajili utungaji wa sera.

Waraka wa Nafasi ya China katika kikao cha 77 cha UNGA ulieleza umuhimu wa kuendeleza jamii ya pamoja yenye umaalum wa usalama kwa wote. Wakati huohuo, ukizungumzia maendeleo ya uchumi kupitia Utekelezaji wa Njia ya Hariri, na kushughulika na maeneo manane muhimu ambayo ni pamoja na usalama wa chakula, ufadhili wa maendeleo, mabadiliko ya tabianchi, uchumi wa kidijitali, na kuondokana na umasikini, kama njia sahihi ya kuongeza kasi ya kutekeleza Ajenda ya mwaka 2030.

Vilevile, chini ya Pendekezo la Usalama wa Dunia lililotolewa na rais wa China Xi Jinping, inawezekana kudumisha malengo na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa ambao utahakikisha utatuzi wa amani wa migogoro yote ya kimataifa na kuboresha usawa na haki kimataifa.

Mwaka huu wa 2023, masuala mengi muhimu ya kimataifa yanahitaji kushughulikiwa kwa haraka. Jamii ya kimataifa inaendelea kukabiliwa na kuongezeka kwa ubaguzi wa rangi, vitendo vya kujilinda kibiashara, umasikini, njaa na migogoro. Ili kukabiliana na haya yote, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linapaswa kuungwa mkono kikamilifu na jamii ya kimataifa ili kuweza kuandaa sera nzuri na zinazoleta matokeo yanayotakiwa.
 
Kama na wewe hujasoma content yote baada ya kujua tu kuwa huu si unga wa ugali wala si ule aliokuwa anajificha nao mzee Manji basi fanya kama unajikuna kwenye likes hapa chini.
 
Back
Top Bottom