mwanawao
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 3,192
- 5,743
Watu wengi wakitaka kuanza kufanya biashara huwa wanaanza kufikiria kuwa na mtaji wa mamilioni shilingi. Katika fikra hizi wengi wa wajasiriamali wamekuwa wakijikuta wakizeeka na ndoto zao bila ya kuzifanyia chochote. Lakini kimtazamo ukiangalia kama ni mtu anataka kufungua biashara ya kuuza bidhaa kwa rejareja (retail business) lazima ataenda kwa wanaouza kwa jumla( whole sale). Anayetaka kuuza kwa whole sale lazima ataenda kiwandani kuchukua bidhaa. Sasa katika chain hii hata kama mtu huna mtaji lakini ukiwa na mtaji wa uaminifu ni rahisi sana kupewa bidhaa husika unayohitaji (kwa kukopeshwa) ukafanya biashara ukapata faida yako na hela ya tajiri ukarudisha.
Nina uhakika hata kwa benki tulizo nazo hapa nchini kama watu wangekuwa ni waamnifu kukopa na kurudisha hela na riba ya benki kama inavyotakiwa leo hii kusingekuwa na haya masharti lukuki yaliyowekwa kwa lengo la kumbana mkopaji.
Kwa wenye viwanda wakiwa waaminifu na kuzalisha bidhaa bora ambazo siyo feki, watajijengea uaminifu kwa wateja wao na bidhaa zao zitakuwa na ushindani mzuri kwenye soko na mitaji yao ingeongezeka kwa haraka.
Leo hii miradi mingi ya uwekezaji ndani ya nchi yetu kama uchimbaji wa madini, utalii, viwanda n.k. ingekuwa inafanywa kwa uaminifu, Taifa letu lingekuwa linatisha katika ukanda huu wa Afrika.
Natamani Watanzania tufikie mahali tuwe waaminifu, tuaminiane, tusaidiane, ili tuweze kuondokana na wimbi hili kubwa la umaskini linalotafuna Taifa letu.
Nina uhakika hata kwa benki tulizo nazo hapa nchini kama watu wangekuwa ni waamnifu kukopa na kurudisha hela na riba ya benki kama inavyotakiwa leo hii kusingekuwa na haya masharti lukuki yaliyowekwa kwa lengo la kumbana mkopaji.
Kwa wenye viwanda wakiwa waaminifu na kuzalisha bidhaa bora ambazo siyo feki, watajijengea uaminifu kwa wateja wao na bidhaa zao zitakuwa na ushindani mzuri kwenye soko na mitaji yao ingeongezeka kwa haraka.
Leo hii miradi mingi ya uwekezaji ndani ya nchi yetu kama uchimbaji wa madini, utalii, viwanda n.k. ingekuwa inafanywa kwa uaminifu, Taifa letu lingekuwa linatisha katika ukanda huu wa Afrika.
Natamani Watanzania tufikie mahali tuwe waaminifu, tuaminiane, tusaidiane, ili tuweze kuondokana na wimbi hili kubwa la umaskini linalotafuna Taifa letu.