Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,925
- Kuna waliofanikiwa kupata utajiri wa pesa na kuwa mamilionea kwa mamilionea kwa ghafla, lakini wengi wao wameishia bankrupt.
- Kuna waliokuwa maskini wameishia kuogelea kwenye utajiri kutokana na mipango mathubuti iliyotokana na ubunifu wao.
Mara kadhaa nimejaribu kuwashauri wengi namna ya kuweza kusimamisha biashara hata kama hana mtaji hata kidogo na kwamba inawezekana, jibu walilonipa ni kwamba bila mtaji haiwezekani, hata ukijaribu kumwelimisha tatizo wamejengeka na hili kwamba kuanza biashara au mradi lazima uwe na mtaji.
- Picha ya kwanza barbashop ya Mzee Vernon Winfrey ambayo amefanya maisha yake yote na ndiyo iliyosaidia kumsomesha Oprah kufikia alipo.
- Picha ya pili Baba mzazi Oprah mzee Vernon Winfrey akiwa na binti yake Opral Winfrey alipofungua barbashop mpya miaka 3-4 hivi iliyopita baada ya kuibomoa ya zamani na kuijenga mpya eneo hilo hilo la uswahilini. Mpaka leo hii anaendelea kufanya kazi hiyo ya kinyozi.
- Picha ya tatu Mzee Vernon Winfrey akiwa kazini kama kinyozi.
Namkumbuka mama mmoja tajiri sana nchini Marekani ambaye ni Oprah Vernon Winfrey, binti ya mzee Vernon Winfrey mwenye barbashop ambaye kwa kipindi fulani alikuwa kinyozi wangu nilipokuwa nchini humo. Barbashop ya babake ndiyo iliyomsomesha Oprah na kisha kuamua kutumia akili yake kwa kulonga kwenye maonyesho ya TV hadi kufikia alipo kuogelea kwenye utajiri. Nyumba alimokulia ambayo imepangishwa kwa wakuja toka Afrika eneo la watu wa daraja ya chini ndipo anayeogelea katika utajiri alimokulia na kusoma shule za watoto maskini.
Wasomi hawana fikra za kujiari bali kuajiriwa
Wahitimu wengi vyuoni wanakazania kuzunguka huku na kule kutafuta kazi, ni dalili za wazi kuwa hawakufundishwa na kufundwa namna na misingi ya kusimama wenyewe ila tu kutegemea ajira. Wengi wanataka njia ya mkato kuwa mamilionea kwa siku moja badala ya subira ya kujenga misingi imara ya kuwawekea dhana ya kukuza uchumi.
Hata tuta la mchicha na viazi ukiwadokezea wanaona kama unafanya utani vile, wakati wangefikiria tuta moja au mawili ya viazi vikikomaa ambavyo huchukua muda mfupi mavuno yake anaweza kupata mtaji wa kuanzisha kiosk cha kusukuma kwa tololi cha kuuza vocha za simu. Mchicha ndio kabisa maana ni wiki mbili hadi tatu unahesabu kitu mkononi, na kwa kuwa ni wasomi wana mbinu za kutafuta soko sehemu zanye pesa kama mahotelini na restaurant, lakini wao wanaona bora kuchakaza kandambili kutembeza Resume kutafuta ajira.
Tujadili namna gani watu wanaweza kutumia elimu yao kusimama wenyewe hasa siku hizi ambapo ajira zinazidi kuwa haba kutokana na wingi wa vyuo na job openings kuwa kama chanda cha dhahabu kwenye kisahani kikikodolewa na maelfu, nani atakipata? Mwenye kukipata itamgharibu zaidi ya kuamua kusimama mwenyewe.