Nikupongeze kijana kwa kuwa na pesa na kuamua ikusaidie kutafuta pesa zaidi
Unapaswa kutambua hakuna biashara isiyokosa changamoto, iwe ndogo au kubwa
Kadiri biashara inavyokuwa kubwa, na changamoto nazo huongezeka
1. Bodaboda
Hakikisha unaandikishiana mkataba na dereva
Hakikisha kunakuwepo na daftari la malipo, kila siku akileta hela anasaini
Hakikisha mkataba unatamka kuwa amalizapo mkataba, pikipiki itakuwa yake, hii huchochea ari ya yeye kuitunza
Hakikisha asipoleta hela hadi ikafika elfu 50, unamnyang'anya pikipiki, zaidi ya hapo huwa hawana uwezo wa kulipa
Usijenge urafiki na dereva, hata akufurahishe vipi, baki kuwa kauzu
Epuka kumtumia yeye akupeleke sehemu za starehe, au akamchukue demu wako au bwana wako mahali
Mahusiano yenu yawe ya kazi tu.
2. Mobile money
Wapo watu wanaouza hizo laini kwa bei chee, nunua hizo, utaelekezwa namna ya kutoa pesa yako kwa urahisi
Uombe mungu usipate tatizo litakalokulazimu uende kwenye kampuni za simu, kwakuwa laini si zako, hutopata msaada isipokuwa mwenye jina lake
Ueke mtu aliyetulia kichwani, anaweza akatumiwa meseji ya kawaida inasomeka mteja katoa hela, kumbe chenga. Yeye akajikuta katoa cash halafu float haijaongezeka. Ndivyo wanavyopigwaga. Awe makini
Anza na mitandao mitatu mikubwa unayoiamini wewe
Usisahau vocha za kurusha na kamashine kaluku
Si lazima fremu hata vile vibox mwake tu au meza na mwamvuli, shega pia
Hakikisha mnaona na huyu mtu kila siku, tena kwa nyakati tofauti, asijue utamuibukia saa ngapi
3. Mitungi ya gas
Ukipata fremu ukaamua kufanya biashara namba 2, basi hata hii utafanya hapohapo
Faida ya mtungi ule mdogo, huwa ni elfu 5, kwa mpya na ule wa kujaza, kama zitapishana si sana, inategemea na kampuni
Unaweza anza na michache, na ukakua polepole
Mtaji wa milioni 2 na nusu unaweza ukakutoa mazima
Eneo lazima liwe ni la makazi ya watu
Weka namba ya simu, wateja wengine wanapenda kupelekewa, akikupigia, unampa bodaboda na namba ya simu ya mteja waelekezane mpaka mtungi umfikie
Hakikisha hakopeshi mtungi
Hakikisha unakaba hadi penati, wanakawaida ya kuongeza mitungi yao, yako hawauzi
Weka namna nzuri ya usimamizi
4.Biashara ya vinywaji baridi
Kama unaweza kupata fremu maeneo kama ya ubungo
Basi nunua freezer, weka maji na soda
Tafuta vijana watakouza kwenye foleni
Utahitaji vijana kama sita, watano wanaizunguka kwenye foleni, na mmoja anaetunza mahesabu
Usisahau kuleta mrejesho kwakile utakachoona ni sawa.
Meflo Mswahili