Mtaji Wa Tsh300,000

Joined
May 8, 2014
Posts
73
Reaction score
10
Habari Wadau Wa Jukwaa La Biashara Na Uchumi.
Nikiwa Na Mtaji Wa 300,000 Naweza Kuanzisha Biashara Gani Kwenye Mikoa Ya Arusha Au Manyara?
 
Anza biashara ya kilimo.. Nunua mashine ya moneymaker water pump kwa ajli ya umwagiliaji, lima angalau ekari 2 zak kuanzia,
nunua mbegu bora za kupandia e.g pannar.. Tafuta eneo lenye chanzo cha maji cha kudumu, anza shughuli za kilimo rasmi..

Au...

Fanyya utafiti juu ya ununuzi wa mahindi sokoni, halafu nunua, saga unga weka kwenye viroba vyenye ujazo kulingana na mahitaji ya wateja wako, ingiza sokoni kwa ajili ya mauzo..
Hapo utakuwa umeongeza thamani ya mahindi na utapata faida kwa kiasi fulani..
Kumbuka sasa hivi kuna njaa kali sana KENYA, hii ni fursa kwako kuwauzia unga wa mahindi..

Ama,

waweza anza kama mnunuzi mdogo wa kuku kutoka maeneo mbali mbali vijijini kwa bei ya chini mfano shs elfu 3.5, halafu unakuja kuwauza mijini kwa bei ya shs 7000 na kuendelea..

Ni wewe tu mkuu kupanga..
Kumbuka mali bila daftari,........
 

ingawa uzi sio wangu ila nimepata kitu kutoka kwako hasa point mbili za mwisho.
 

Mkuu nimepata ujumbe wako kwa ufasaha.
 

Ubarikiwe ndugu, mawazo yako ni yakawaida sana, kiasi kwamba hamshindi mtanzania wa kawaida.

Nashukuru maana nimefaidika.
 
Mfano kijiji gani mkuu!!
tuze nasi tupate tujichanganye!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…