Mtalaa vs Mtaala!

Mtalaa vs Mtaala!

Mtumishi Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2011
Posts
259
Reaction score
92
Wataalamu, kwa muda sasa nimekuwa nikisoma kwenye magazeti yetu wanaandika mitalaa. Kwa ufahamu wangu ninajua kuwa ni mitaala na sio mitalaa, ila kwa jinsi matumizi ya neno mitalaa yanavyoongezeka nikahisi labda mimi ndio nakosea, ni neno lipi sahihi kati ya mitalaa na mitaala? Asanteni
 
Wataalamu, kwa muda sasa nimekuwa nikisoma kwenye magazeti yetu wanaandika mitalaa. Kwa ufahamu wangu ninajua kuwa ni mitaala na sio mitalaa, ila kwa jinsi matumizi ya neno mitalaa yanavyoongezeka nikahisi labda mimi ndio nakosea, ni neno lipi sahihi kati ya mitalaa na mitaala? Asanteni

it seems we ar not serious na selikali yetu.
 
Wataalamu, kwa muda sasa nimekuwa nikisoma kwenye magazeti yetu wanaandika mitalaa. Kwa ufahamu wangu ninajua kuwa ni mitaala na sio mitalaa, ila kwa jinsi matumizi ya neno mitalaa yanavyoongezeka nikahisi labda mimi ndio nakosea, ni neno lipi sahihi kati ya mitalaa na mitaala? Asanteni

neno sahihi la kiswahili ni mitalaa.
 
Mimi najua mitaala, inayotoka katika msingi mmoja na taaluma, yenye wataalamu.

Mitalaa sijawahi kuisikia, labda kama ni neno jipya au sikulijua.
 
Mimi najua mitaala, inayotoka katika msingi mmoja na taaluma, yenye wataalamu. Mitalaa sijawahi kuisikia, labda kama ni neno jipya au sikulijua.
Kamusi ya kiswahili:TUKI (2001) ina neno MTALAA (kwa maana ya curriculum) na sio MTAALA!
 
Kamusi ya kiswahili:TUKI (2001) ina neno MTALAA (kwa maana ya curriculum) na sio MTAALA!

Mtalaa na mtaala yote ni sahihi.

Ila mtalaa lina maana mbili zaidi, nazo ni; (1)kusoma na (2)kujifunza.

Mtaala maana yake ni moja tu.

Hivyo, kwa mujibu wa TUKI chapa ya Tano, 2010, neno mtalaa lina maana tatu na mojawapo ikiwa ndiyo hiyo ya curriculum.
 
... Ndiyo' "MTALAA" ni (study, reading, curriculum )
... "MTAALA" ni (curriculum)
 
Yote sahihi...... muulize Mulugo uone kama anajua!
 
Hivi Mbatia alitaka aone tu mtalaa au alitaka iboreshwe ili elimu iendane na mahitaji ya msingi ya jamii ya ki-Tz? Nauliza kwani nasikia baada ya kugawa nakala za mitaala basi hoja imefungwa.
 
Ukiangalia vizuri katika Kamusi ya Kiswahili sanifu iliyoandikwa na TUKI,neno la kiswahili lililotumika kutoa kiswahili cha neno "Curriculum" ni Mtaala, na sio Mtalaa kama wandishi wa magazeti wanavyoliandika. Nafikiri hawa wandishi wa magazeti watakuwa nao hawajui neno sahihi la kiswahili linalomaanisha "Curriculum". Warudi shuleni/vyuoni wakajifunze upya.
 
Back
Top Bottom