Elections 2010 Mtangazaji Clouds Zamaradi Mketema kuwania Ubunge

Elections 2010 Mtangazaji Clouds Zamaradi Mketema kuwania Ubunge

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2009
Posts
5,471
Reaction score
752
0705+Dikololo+006.jpg


Na Mwandishi Wetu
Mtangazaji anayekuja kwa kasi kwenye ‘field’ hiyo Zamaradi Nketema ambaye anapiga mzigo katika Kituo cha Radio Clouds Fm, naye ameamua kwa moyo mmoja kuingia kwenye siasa huku kiu yake ikiwa ni kutinga Bungeni baadaye Novemba mwaka huu.

Juzi, Jumanne Amani lilitumiwa ujumbe mfupi na chanzo chake makini, kikitonya kwamba: “Oyaaa Zamaradi amechukua fomu ya kugombea Ubunge kupitia Viti Maalum – CCM.”

Kama kawa, bila kuchelewa Askari wa Amani alimvutia waya Zamaradi na kutaka kujua ukweli wa stori hiyo ambapo alitoa ushirikiano wa kutosha.

“Ni kweli nimechukua fomu leo (Jumanne) na ninatarajia kurudisha kesho. Siwezi kuongea mengi kwasasa, labda hadi nitakaporudisha fomu. Nitafute kuanzia kesho (Jumatano) na kuendelea, ninaweza kuwa na mengi ya kuongea,” alisema Zamaradi.

Zamaradi anakuwa Mtangazaji wa pili wa kituo hicho kurusha karata yake kwenye kinyang’anyiro hicho baada ya marehemu Amina Chifupa kufanikiwa kuingia bungeni kwa uteuzi kama anaowania.

SOURCE: GBL
 
Wishing her Lucky..
But Amina was Amina...
 
Aanze basi kuvaa kwa nidhamu asionyeshe kifua!! Akumbuke ubishoo huo Amina uliwahi kumtoa nje ya Bunge baada ya kuvaa ndivyosivyo. Tunajua anaweza lakini aache kuvaa vinguo vya watoto. Zaidi ya hayo kila la kheli.
 
..she luks too young kuwa na majukumu...all the best lakini...
 
Unamaanisha huyu hapa kwenye picha!
Aiseee!

Picture+008.jpg
Akumbuke kuna akina watu kama akina Kabwe................. huwa wanakula sahani moja na watu kama hawa.................. Amina Chifupa si ndo alikuwa wa namna hii na alitoka Redio hiyo hiyo
 
Namuonea huruma akifanikiwa kuingia bungeni na kukutana na kina Nchimbi sijui kama atasalimika.
 
Unamaanisha huyu hapa kwenye picha!
Aiseee!

Picture+008.jpg

Anajua kwanza Nini maana ya Bunge, nini kazi za Mbunge! Je anajua Mfumo wa Taifa letu? Naamini kabisa kuna Wabunge wengi hawafahamu kwamba Bunge ni Mhimili wenye Nguvu kama ilivyo Serikali na Mahakama
 
Curiosity has its own reason to exist..labda anajua fika nini anachoomba kukifanya. Vinginevyo bunge si kipindi cha sinema au leo tena, Lol
 
Hivi watu wengi wanao enda bungeni wana jua katiba na sheria za nchi? Sio huyu tu bali wengi wao kwa ujumla.
Naunga mkono kwa vijana kuwa part of the changes ,ila kwa kijana kujua mengi inabidi awe katumia muda wake vizuri kufanya her/his home work .
just curiosity.Otherwise I wish her the best.
 
ama kweli ubunge sasa unataka kuwa kichekesho, hivi huyu wa darasa la nne pale clouds FM awe naye mbunge lahaulaa usishangae na kibonde nae akataka kugombea ubunge, wao wakae na clouds yao kupiga umbea we need serios people in the parliament katika kipindi hiki tunachotaka mabadiliko ya kweli tanzania na sio wauza sura kama hawa comedians wa clouds FM.
 
Back
Top Bottom