Mtangazaji wa Wasafi FM, Gerald Hando ataka mtandao wa TIkTok ufungiwe Tanzania

Mtangazaji wa Wasafi FM, Gerald Hando ataka mtandao wa TIkTok ufungiwe Tanzania

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mtangazaji wa kipindi cha Goodmoring cha Wasafi FM Gerald Hando ametaka au kushauri mtandao wa TikTok Tanzania ufungiwe akidai unaleta matatizo ya afya ya akili kwa vijana wengi zaidi.

Amesema vijana sasa wakilala wakiamka wanawaza wapata bando ili waingie TikTok wafanye mambo yao na akikosa bando yupo tayari apoteze heshima na utu wake ili apate bando tu.

Hii imekaaje jamani mbona kuna harakati nyingine hazina afya kabisa. Kama kuna changamoto ni bora wakasema ziweke sawa kuliko kufikia hatua ya kutaka kufungia mtandao husuki.

Maana kwa sasa mitandao hii ya kijamii kiukweli kabisa imekuwa sehemu ya ajira kwa vijana wengi sana so akitokea mtu anaeta hoja kama hii bila shaka vijana wanaweza wakampiga spana nzito kwa hoja yake hiyo.

Soma Pia:
Hivi karibuni tuliona kuna kampeni ya kutaka kufungiwa kwa mtandao wa X( Twitter) ambayo ilichukuliwa kama ajenda fulani hadi kwenye vyama vya kisiasa na hata upande pia wa baadhi ya viongozi wa dini wakichochea fulani hivi X ufungiwe Tanzania.

 
Mtangazaji wa kipindi cha Goodmoring cha Wasafi FM Gerald Hando ametaka au kushauri mtandao wa TikTok Tanzania ufungiwe akidai unaleta matatizo ya afya ya akili kwa vijana wengi zaidi.
Ni upuuzi, changamoto wabongo atujaandaliwa kuishi kwenye dunia ya ushindani. Maudhui ya wabongo "kuonyesha makario", "Kuonyesha maisha feki","Washauri wa ndoa na mapenzi wasiokuwa na vyeti" na ujinga mwingine. Angalia wachina wakike na wakiume; wanatangaza biashara, historia ya nchi yao na vitu vya kiutamaduni. Kwann ufungiwe kwa udhaifu wako we mbongo
 
Huyu geradi na wenzake wanaoendesha kile kipindi wanajiona ni watu muhimu sana nchi hii wanadhani wanaweza kuinfluence chochote kwa midomo yao. Tiktok ni mtandao useful sana inategemea na mtumiaji
 
Mtangazaji wa kipindi cha Goodmoring cha Wasafi FM Gerald Hando ametaka au kushauri mtandao wa TikTok Tanzania ufungiwe akidai unaleta matatizo ya afya ya akili kwa vijana wengi zaidi.

Amesema vijana sasa wakilala wakiamka wanawaza wapata bando ili waingie TikTok wafanye mambo yao na akikosa bando yupo tayari apoteze heshima na utu wake ili apate bando tu.

Hii imekaaje jamani mbona kuna harakati nyingine hazina afya kabisa. Kama kuna changamoto ni bora wakasema ziweke sawa kuliko kufikia hatua ya kutaka kufungia mtandao husuki.

Maana kwa sasa mitandao hii ya kijamii kiukweli kabisa imekuwa sehemu ya ajira kwa vijana wengi sana so akitokea mtu anaeta hoja kama hii bila shaka vijana wanaweza wakampiga spana nzito kwa hoja yake hiyo.

Soma Pia: Ushauri wa Gerald Hando kuhusu tiktok ni mwiba kwa uhuru

Hivi karibuni tuliona kuna kampeni ya kutaka kufungiwa kwa mtandao wa X( Twitter) ambayo ilichukuliwa kama ajenda fulani hadi kwenye vyama vya kisiasa na hata upande pia wa baadhi ya viongozi wa dini wakichochea fulani hivi X ufungiwe Tanzania.

Ana hela za kuwalipa creators wa bongooo
 
Kuna watu wana uwezo mdogo wa kufikiri mithili ya chembe ya haradali.
 
Hii imekaaje jamani mbona kuna harakati nyingine hazina afya kabisa. Kama kuna changamoto ni bora wakasema ziweke sawa kuliko kufikia hatua ya kutaka kufungia mtandao husuki.
Tatizo siyo TikTok
Shida iko kwenye elimu yetu haimjengi mtu kujitambua
 
Kuna nchi zimepiga marufuku kabisa mtandao huu kama India na hata Somalia na Nepal
Na nchi kama za ulaya na 🇺🇸 wamepiga marufuku baadhi ya watu kutumia kama mashirika ya Umma na maofisi mengi tu ila sio marufuku kwingine

Mtandao wowote ukitaka kujifunza vitu vingi sana na hata kupata elimu ya vitu unapata humo
Wengi wamejifunza maujanja hata ya mapishi ya dunia na hata ujenzi na ufundi
Wengine wamepata fursa nyingi sana huko
Ila kama unataka siku nzima uangalie upumbafu wa vile vicheko hata mtu akitumbukia kwenye msingi kalewa
Basi mtu anahangaika siku nzima kwa ujinga
 
Huyu geradi na wenzake wanaoendesha kile kipindi wanajiona ni watu muhimu sana nchi hii wanadhani wanaweza kuinfluence chochote kwa midomo yao. Tiktok ni mtandao useful sana inategemea na mtumiaji
Sana tena, wakikaa pamoja wakiwa wanapiga mikelele wanajikuta ni kama jopo la watunga sheria wa nchi hii.
 
ni moja ya mtandao wa ovyo sana, wengi wa wadau wake ni watu walipanguka akili kiaina, binafasi nimechoka kugomabana na mwenza wangu, haelewi kabisa anaweza akasamehe kula hela akaunga bando kwa ajili ya tiktok
 
Back
Top Bottom