Mzalendo_Mkweli
JF-Expert Member
- Jan 30, 2012
- 2,025
- 1,270
Kiungo wa SK Sturm Graz, Mtanzania Michael Lema amesema anajivunia kupata nafasi ya kucheza dhidi ya kiungo wa Ghana na West Ham, Andre Ayew.
Katika mchezo huo wa maandalizi ya mwanzo wa msimu uliofanyika kwenye Uwanja wa Thermenstadio ulishudia timu hizo zikitoka suluhu.
Lema alisema Ayew ni moja ya mastaa wa Afrika wanaomvutia na mara baada ya mchezo huo aliona ni bora kuzungumza na nyota wa Ghana.
“Nilimwendea na kujitambulisha kwake alinichangamkia na nilimuomba aniambie jambo ambalo linaweza nisaidia kwenye soka langu, alitabasamu na kuniambia kuwa hakuna linaloshindikana penye nia," alisema kinda huyo.
Katika mechi hiyo Lema alicheza katika dakika zote tisini na kupambana na mabeki Pablo Zabaleta na Sam Byram wa West Ham.
Source : Mtanzania ajivunia kucheza Ayew
Player Profile : Michael John Lema - Spielerprofil 17/18
Katika mchezo huo wa maandalizi ya mwanzo wa msimu uliofanyika kwenye Uwanja wa Thermenstadio ulishudia timu hizo zikitoka suluhu.
Lema alisema Ayew ni moja ya mastaa wa Afrika wanaomvutia na mara baada ya mchezo huo aliona ni bora kuzungumza na nyota wa Ghana.
“Nilimwendea na kujitambulisha kwake alinichangamkia na nilimuomba aniambie jambo ambalo linaweza nisaidia kwenye soka langu, alitabasamu na kuniambia kuwa hakuna linaloshindikana penye nia," alisema kinda huyo.
Katika mechi hiyo Lema alicheza katika dakika zote tisini na kupambana na mabeki Pablo Zabaleta na Sam Byram wa West Ham.
Source : Mtanzania ajivunia kucheza Ayew
Player Profile : Michael John Lema - Spielerprofil 17/18