MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Leo tarehe 23/02/2025 huko nchini Korea Kusini bendera ya taifa imepeperushwa vyema na kijana Mtanzania Gabriel Geay kwa kuvunja rekodi ya mbio za Daegu Marathon (course record) kwa kutumia muda wa masaa 2:05:20 na kuibuka wa kwanza. Ikumbukwe Geay ndo anashikilia rekodi ya taifa ya marathon kwa muda wa masaa 2:03:00 kupitia Valencia Marathon ya mwaka 2022. Hapo chini nimekuwekea matokeo ya nane bora.
Daegu Marathon 2025 results (top eight):
Men's elite race
Gabriel Geay (TAN) 2:05:20
Addisu Gobena (ETH) 2:05:22
Dejene Megersa (ETH) 2:05:59
Ogbe Kibrom Ruesom (ERI) 2:06:04
Othmane El Goumri (MAR) 2:06:07
Gilbert Kibet (KEN) 2:06:39
Stephen Kiprop (KEN) 2:07:16
Sezgin Atac (TUR) 2:07:26
Geay ni mfano wa kuigwa miongoni mwa wanamichezo wa taifa hili. Huyu ni miongoni mwa wanamichezo wachache sana wasomi hapa nchini. Nje ya riadha nafurahishwa mno na jinsi anavyorudisha kwa jamii kupitia riadha. Siku za hivi karibuni ameanzisha charity organisation inayojulikana kama Geay Foundation kwa nia ya kusaidia mambo mbalimbali hasa kuinua vipaji vya watoto wenye vipaji vya michezo. Yuko tofauti na wanamichezo wengine wanaorudisha kwa jamii kwa kujenga misikiti na makanisa badala ya kusaidia fani zilizowainua wao.
Ninatarajia hakutakuwa na mizengwe kwenye hii foundation yake ili taifa linufaike. Miaka iliyopita kulikuwa na shirika la Shoe 4 Africa from America lililokuwa linasapoti mambo ya riadha ila walishindwana na wabongo wakaamua kuweka nguvu Kenya ambako hadi leo wanafanya makubwa. Unaweza ku-google kuhusu Shoe 4 Africa.
Daegu Marathon 2025 results (top eight):
Men's elite race
Gabriel Geay (TAN) 2:05:20
Addisu Gobena (ETH) 2:05:22
Dejene Megersa (ETH) 2:05:59
Ogbe Kibrom Ruesom (ERI) 2:06:04
Othmane El Goumri (MAR) 2:06:07
Gilbert Kibet (KEN) 2:06:39
Stephen Kiprop (KEN) 2:07:16
Sezgin Atac (TUR) 2:07:26
Geay ni mfano wa kuigwa miongoni mwa wanamichezo wa taifa hili. Huyu ni miongoni mwa wanamichezo wachache sana wasomi hapa nchini. Nje ya riadha nafurahishwa mno na jinsi anavyorudisha kwa jamii kupitia riadha. Siku za hivi karibuni ameanzisha charity organisation inayojulikana kama Geay Foundation kwa nia ya kusaidia mambo mbalimbali hasa kuinua vipaji vya watoto wenye vipaji vya michezo. Yuko tofauti na wanamichezo wengine wanaorudisha kwa jamii kwa kujenga misikiti na makanisa badala ya kusaidia fani zilizowainua wao.
Ninatarajia hakutakuwa na mizengwe kwenye hii foundation yake ili taifa linufaike. Miaka iliyopita kulikuwa na shirika la Shoe 4 Africa from America lililokuwa linasapoti mambo ya riadha ila walishindwana na wabongo wakaamua kuweka nguvu Kenya ambako hadi leo wanafanya makubwa. Unaweza ku-google kuhusu Shoe 4 Africa.