Mtazamo;Unapoingia mwaka mpya na kutimiza miaka kadhaa unatakiwa usikitike na kutafakari nyakati zako na sio kusherekea......

Mtazamo;Unapoingia mwaka mpya na kutimiza miaka kadhaa unatakiwa usikitike na kutafakari nyakati zako na sio kusherekea......

KikulachoChako

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2013
Posts
19,185
Reaction score
37,239
Habari za muda huu waungwana.....

Mimi nadhani maisha ya kiumbe mwanadamu hapa duniani yamekuja mfano wa simu iliyojaa chaji na kutolewa kwenye chaji pindi anapozaliwa kutoka tumboni kwa mama yake.......

Na chaji hutumika na kupungua kwa kadri anavyoziiishi nyakati zake hapa duniani.....na bahati mbaya hakuna kuongeza chaji badala ni kutumia chaji...

Kwa muktadha huo ni kuwa iko siku chaji itaisha na kuzimika kwa kadri mola wake alivyo mkadiria......

Kiuhalisia ni kuwa kwa kadri unavyoziishi nyakati zako ndivyo unavyozikaribia siku za agano lako na mola wako za kuishi juu ya mgongo wa ardhi.......

Hekima ni kuwa kila inapokupita nyakati unatakiwa kukaa na kutafakari ya nyuma na kuyarekebisha huku ukiziishi vyema nyakati zijazo ili kuwa na mwisho mwema........

Muungwana hawezi kushangilia kuisha kwa chaji kwenye simu yake hali ya kuwa hana uwezo wa kupata chaji nyingine bali hutafakari na kuitumia vyema chaji kidogo iliyobakia ambayo pia inaendelea kuisha.......

Tujitahidi kuziishi nyakati zetu vyema kwa kadri tulivyobarikiwa huku tukijua kuwa iko siku chaji yetu itakwisha na tutazima(kufariki).......

Hata tuliowazika nao walikuwa watu kama sisi, wenye mipango na mikakati kama sisi na pengine hawakuwa wanajua kuwa wanaziishi nyakati zao za mwisho kwani umauti huja ghafla......

Najua taarifa hii inaweza isiwe ya kupendeza kwa watu walio wengi lakini wanadamu ni vyema kukumbushana kwani kujisahau ni maumbile yetu.......

Nawasilisha......
 
Habari za muda huu waungwana.....

Mimi nadhani maisha ya kiumbe mwanadamu hapa duniani yamekuja mfano wa simu iliyojaa chaji na kutolewa kwenye chaji pindi anapozaliwa kutoka tumboni kwa mama yake.......

Na chaji hutumika na kupungua kwa kadri anavyoziiishi nyakati zake hapa duniani.....na bahati mbaya hakuna kuongeza chaji badala ni kutumia chaji...

Kwa muktadha huo ni kuwa iko siku chaji itaisha na kuzimika kwa kadri mola wake alivyo mkadiria......

Kiuhalisia ni kuwa kwa kadri unavyoziishi nyakati zako ndivyo unavyozikaribia siku za agano lako na mola wako za kuishi juu ya mgongo wa ardhi.......

Hekima ni kuwa kila inapokupita nyakati unatakiwa kukaa na kutafakari ya nyuma na kuyarekebisha huku ukiziishi vyema nyakati zijazo ili kuwa na mwisho mwema........

Muungwana hawezi kushangilia kuisha kwa chaji kwenye simu yake hali ya kuwa hana uwezo wa kupata chaji nyingine bali hutafakari na kuitumia vyema chaji kidogo iliyobakia ambayo pia inaendelea kuisha.......

Tujitahidi kuziishi nyakati zetu vyema kwa kadri tulivyobarikiwa huku tukijua kuwa iko siku chaji yetu itakwisha na tutazima(kufariki).......

Hata tuliowazika nao walikuwa watu kama sisi, wenye mipango na mikakati kama sisi na pengine hawakuwa wanajua kuwa wanaziishi nyakati zao za mwisho kwani umauti huja ghafla......

Najua taarifa hii inaweza isiwe ya kupendeza kwa watu walio wengi lakini wanadamu ni vyema kukumbushana kwani kujisahau ni maumbile yetu.......

Nawasilisha......
MKUUU UKO SAHIHI, HATA MIMI NAWASHANGAAA SANA HAWA WANAOSHANGILIA MWAKA MPYA , SIJUI WANASHANGILIA NINI WAKATI MUDA WA KIFO NDO UNAKARIBIA
 
MKUUU UKO SAHIHI, HATA MIMI NAWASHANGAAA SANA HAWA WANAOSHANGILIA MWAKA MPYA , SIJUI WANASHANGILIA NINI WAKATI MUDA WA KIFO NDO UNAKARIBIA

“Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.

— Ufunuo wa Yohana 14:13 (Biblia Takatifu)
 
Habari za muda huu waungwana.....

Mimi nadhani maisha ya kiumbe mwanadamu hapa duniani yamekuja mfano wa simu iliyojaa chaji na kutolewa kwenye chaji pindi anapozaliwa kutoka tumboni kwa mama yake.......

Na chaji hutumika na kupungua kwa kadri anavyoziiishi nyakati zake hapa duniani.....na bahati mbaya hakuna kuongeza chaji badala ni kutumia chaji...

Kwa muktadha huo ni kuwa iko siku chaji itaisha na kuzimika kwa kadri mola wake alivyo mkadiria......

Kiuhalisia ni kuwa kwa kadri unavyoziishi nyakati zako ndivyo unavyozikaribia siku za agano lako na mola wako za kuishi juu ya mgongo wa ardhi.......

Hekima ni kuwa kila inapokupita nyakati unatakiwa kukaa na kutafakari ya nyuma na kuyarekebisha huku ukiziishi vyema nyakati zijazo ili kuwa na mwisho mwema........

Muungwana hawezi kushangilia kuisha kwa chaji kwenye simu yake hali ya kuwa hana uwezo wa kupata chaji nyingine bali hutafakari na kuitumia vyema chaji kidogo iliyobakia ambayo pia inaendelea kuisha.......

Tujitahidi kuziishi nyakati zetu vyema kwa kadri tulivyobarikiwa huku tukijua kuwa iko siku chaji yetu itakwisha na tutazima(kufariki).......

Hata tuliowazika nao walikuwa watu kama sisi, wenye mipango na mikakati kama sisi na pengine hawakuwa wanajua kuwa wanaziishi nyakati zao za mwisho kwani umauti huja ghafla......

Najua taarifa hii inaweza isiwe ya kupendeza kwa watu walio wengi lakini wanadamu ni vyema kukumbushana kwani kujisahau ni maumbile yetu.......

Nawasilisha......
Kufa ni sherehe kwa wengine kuwa wamemaliza safari maana unajua tu kuwa utakufa na kila mtu atakufa. Hivyo hupaswi kuogopa. It's like graduating—who doesn't love graduating?
 
Ukiwa unawaza ya mbele always, utakata tamaa na kuona maisha hayana thamani. Tafuta maisha, enjoy maisha ..... Mengine yatajisumbukia yenyewe. Kifo kipo tu hata unune ama ucheke
 
Kufa ni sherehe kwa wengine kuwa wamemaliza safari maana unajua tu kuwa utakufa na kila mtu atakufa. Hivyo hupaswi kuogopa. It's like graduating—who doesn't love graduating?
Sijasema kuwa unapaswa kuogopa kufariki bali kutafakari na kujiandaa na maisha baada ya kifo( kwa wenye Imani)
 
Unabidi uanze mbele ndo urudi nyuma hii ndo Asili ya MAISHA.

Wanaosherekea kuumaliza mwaka ni wale ambao walianzia nyuma na kwenda mbele .

Japo yote ni mitazamo sahihi.

Ila miaka inavyozidi kwenda ndo unavyozidi kurudi ulipokuwa mwanzo.
 
Unabidi uanze mbele ndo urudi nyuma hii ndo Asili ya MAISHA.

Wanaosherekea kuumaliza mwaka ni wale ambao walianzia nyuma na kwenda mbele .

Japo yote ni mitazamo sahihi.

Ila miaka inavyozidi kwenda ndo unavyozidi kurudi ulipokuwa mwanzo.
Hakika ndugu.....
 
Ukiwa unawaza ya mbele always, utakata tamaa na kuona maisha hayana thamani. Tafuta maisha, enjoy maisha ..... Mengine yatajisumbukia yenyewe. Kifo kipo tu hata unune ama ucheke
Kila mwenye Imani anatambua uwepo wa kifo....na kila mwenye kutambua uwepo wa kifo kwa njia ya imani anatambua kuna maisha baada ya kifo na siku ya hukumu.....ubora au ubaya siku yako ya hukumu unaletwa na matendo yako ukiwa hai maana mtu mfu ameshamaliza ya kwake......kuishi ni kutokana na agano lako na mola wako mlezi kwa mujibu wa mlango wa Imani
 
Unabidi uanze mbele ndo urudi nyuma hii ndo Asili ya MAISHA.

Wanaosherekea kuumaliza mwaka ni wale ambao walianzia nyuma na kwenda mbele .

Japo yote ni mitazamo sahihi.

Ila miaka inavyozidi kwenda ndo unavyozidi kurudi ulipokuwa mwanzo.
sawa dr.
 
Back
Top Bottom