Mtazamo wangu kama Azam FC ingekuwa chini ya Macio Maximo.

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,703
Reaction score
1,724
Mafanikio tuliyoyapata kwenye timu yetu ya taifa chini ya kocha Macio Maximo hayatasahaulika. Lilikuwa kosa la kiufundi kwa kocha huyo kukubali kuifundisha Yanga, ila kama Azam FC walipoachana na kocha Joseph Omog wangemuajiri Maximo kwa kweli timu yetu sasa hivi ingekuwa inacheza soka la uhakika. Hata hivo benchi la sasa la ufundi naliamini litatuletea soka murua na la ushindi. Mungu ibariki Azam FC leo na siku zote. Amen.
 
AZAM FC IDUMU ZAIDI,jamaa wanasakata mpira leo,simba atageuka paka so muda!
 
Azam ,azam ,azam kitu gani bana,acheni kutyzingua kama mnalambishwa ice cream tulieni huko huko.
 
AZAM FC IDUMU ZAIDI,jamaa wanasakata mpira leo,simba atageuka paka so muda!
Mkuu, matokeo yamenifanya T-Shirt yake niifue japo toka niifungue ilikuwa siku ya tatu tu.
 
Sidhani mkuu kwani kazi aliyokuwa akiifanya kwenye timu yetu ya taifa sawasawa na kocha wa klabu ndo maana Yanga wakafanya mizengwe ili ajiunge nao. Pale uswahili mwingi asingeweza @ Belo.
 
Sidhani mkuu kwani kazi aliyokuwa akiifanya kwenye timu yetu ya taifa sawasawa na kocha wa klabu ndo maana Yanga wakafanya mizengwe ili ajiunge nao. Pale uswahili mwingi asingeweza @ Belo.

Maximo Stars alikuwa anacheza defensive game na ilimsaidia kwani aliikuta timu kwenye hali mbaya,game nyingi Stars ilikuwa underdog so kucheza defensive ilimsaidia na Stars ikapanda.Azam/Yanga ni timu kubwa hupaswi kucheza defensive game unapaswa kushambulia upate matokeo ndio maana alichemsha Yanga na hata Azam ingemshinda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…