Mti wa Mvule au "Milicia exelecia" ni mti wa mbao

Mti wa Mvule au "Milicia exelecia" ni mti wa mbao

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1624162065787.jpeg

Jina lingine ni iroko. Ni mti wenye mbao imara ambazo pia hard wood. Unapatikana Afrika kwenye misitu ya mwambao wa bahari kutoka Benin mpaka Angola, Msumbiji Lamu Madagascar.

Inasadikika miti hii inafuga mashetani, kule Benini sadaka hutolewa chini ya mti huu hasa kwa wenye matatizo ya uzazi.

Unaweza kurefuka kufikia mita 50 au futi 160. Maajabu ya mti huu huwa miwili jike na dume pamoja. Dume hutoa mbelewe zinazojifunga kwenye majani ya jike. Jike hutoa maua kati ya mwezi December na January. Baada ya maua hutoa jamii ya nuts zinazopendwa kuliwa na nguchiro, popo au ndege. Hawa ndiyo wasambazaji wakuu wa mbegu za mvule.

Kutokana na ubora wa mbao ndiyo nilifuatilia uwezekano wa kuotesha mitii shambani kwangu. Katika utafiti niliyo ufanya, mbegu zinazoweza kuota ni zile zilizopita tumboni mwa viumbe nilivyo vitaja hapo juu. Mvule ukiwa mchanga haupendi mwanga wa jua na unapenda unyevu nyevu.

Baada ya kipindi cha uchanga kuisha Mvule unaweza kustahilimili ukame mradi mizizi yake ifikie maji chini ya ardhi. Ndiyo maana inastawi katika misitu ya pwani kwenye high water table.

Miti hii ipo hatarini kupotea duniani na ni moja ya miti inayohifadhiwa na UNESCO
 
Eti hata mibuyu nayo kuna maneno yanasemwa inafuga majini? Mbuyu jiti kubwaa lakini hasara tu ukiacha matunda yake hata kibao cha kukalia hupati acha mbao sasa.
 
Miche ya mti huu inaweza kupatikana kwa wauzaji wa kawaida?
 
Back
Top Bottom