Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 753
- 1,812
MMOJA ya watia wa jimbo la Arumeru Magharibi, Ezekiel Elphas Mollel amejitosa kumuunga mkono mgombea mteule wa CCM, Noar Lembriss Mollel akidai ni operesheni kabambe ya kulikomboa jimbo hilo lililopo chini ya upinzani na kulirejesha CCM ambapo amewaomba wanaCCM pia kuwa wamoja katika kumwombea kura Rais John Magufuli.
Akiongea na vyombo vya habari Ezekiel ambaye alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa watiania 61 wa jimbo hilo amekipongeza chama cha mapinduzi kwa kumteua Noar Lembris akidai kwamba uamuzi huo unapaswa kuzingatiwa na wanaccm kwani zamu yake bado na kuwataka kumuunga mkono mgombea huyo.
Ezekiel amekuwa kada wakwanza kujitokeza hadharani kumuunga mkono mteuli huyo Lembris Noar ambaye aliwahi kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha kupitia Chama cha Chadema kabla hajahamia CCM, akidai kuwa nia yake ya dhati ni kuona jimbo la Arumeru masharibi linatoka upinzani .
Ezekiel ambaye kitaaluma ni Mwalimu,amesema yupo tayari kusubiri wakati mwingine wa kuwania nafasi ya ubunge ila kwa sasa itoshe kusema kwamba nguvu yetu ni kukomboa jimbo letu la Arumeru Magharibi"
Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Chadema chini ya mbunge aliyemaliza muda wake Gibson Ole Meseiyeki ambaye amepata tena uteuzi wa kupeperusha bendera ya Chadema .
Akiongea na vyombo vya habari Ezekiel ambaye alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa watiania 61 wa jimbo hilo amekipongeza chama cha mapinduzi kwa kumteua Noar Lembris akidai kwamba uamuzi huo unapaswa kuzingatiwa na wanaccm kwani zamu yake bado na kuwataka kumuunga mkono mgombea huyo.
Ezekiel amekuwa kada wakwanza kujitokeza hadharani kumuunga mkono mteuli huyo Lembris Noar ambaye aliwahi kuwa mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha kupitia Chama cha Chadema kabla hajahamia CCM, akidai kuwa nia yake ya dhati ni kuona jimbo la Arumeru masharibi linatoka upinzani .
Ezekiel ambaye kitaaluma ni Mwalimu,amesema yupo tayari kusubiri wakati mwingine wa kuwania nafasi ya ubunge ila kwa sasa itoshe kusema kwamba nguvu yetu ni kukomboa jimbo letu la Arumeru Magharibi"
Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Chadema chini ya mbunge aliyemaliza muda wake Gibson Ole Meseiyeki ambaye amepata tena uteuzi wa kupeperusha bendera ya Chadema .