jamesmwakalinga
Member
- Oct 17, 2024
- 6
- 7
Hali si swari ndani ya chama cha mapinduzi(CCM)jimbo la moshi mjini ambako kada wa chama hicho na mtia nia wa kiti cha ubunge hapo mwakani kumporomoshea matusi mstahiki meya wa Manipsaa ya moshi,Zuberi kidumo.
Taflani hiyo imezuka leo asubuhi nje ya jengo la ofisi za CCM Moshi mjini ambako Ibrahim Shayo anayetajwa kuonesha nia ya kuwania ubunge hapo mwakani kuzua zogo.
Zogo hilo lilizuka muda mfupi baada ya wawili hao kutoka ndani ya kikao ambacho kiliitishwa na mwenyekiti wa ccm moshi mjini,Faraj Swai.
Haikujulikana mara moja kikao hicho kilikuwa na agenda gani kutokana na kuhusisha baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya akiwamo mkuu wa wilaya,mkuu wa polisi wa wilaya(OCD)mku wa usalama wa taifa wa wilaya(DSO),mbunge wa jimbo la moshi mjini,Priscus Tarimo,mstahiki meya wa manispaa ya moshi,Zuberi Kidumo na katimu wa ccm wa wilaya.
"Wewe nenda hapo kwenye jengo la ccm wilaya,mtafute fundi anaitwa.........,huuyo atakueleza vizuri maana ndiyo aliyeshuhudia mtia nia akimporomoshea matusi mstahiki meya",amesema mtoa taarifa wetu aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Mmoja wa wajumbe aliyehudhulia kikao hicho hakuwa tayari kuelezea kilichojadiliwa ndani ya kikoa hicho na kuomba atafutwe mwenyekiti wa ccm moshi mjini,faraj Swai mabaye hata hivyo simu yake iliita bila majibu.
Soma Pia: Siasa za kuchafuana zashika kazi CCM Moshi mjini
Nini chanzo cha kada huyo kuvurumisha matusi kwa meya wake,fuatilia ukurasa huu hapo baadae tutaweeka kila kitu.
Taflani hiyo imezuka leo asubuhi nje ya jengo la ofisi za CCM Moshi mjini ambako Ibrahim Shayo anayetajwa kuonesha nia ya kuwania ubunge hapo mwakani kuzua zogo.
Zogo hilo lilizuka muda mfupi baada ya wawili hao kutoka ndani ya kikao ambacho kiliitishwa na mwenyekiti wa ccm moshi mjini,Faraj Swai.
Haikujulikana mara moja kikao hicho kilikuwa na agenda gani kutokana na kuhusisha baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya akiwamo mkuu wa wilaya,mkuu wa polisi wa wilaya(OCD)mku wa usalama wa taifa wa wilaya(DSO),mbunge wa jimbo la moshi mjini,Priscus Tarimo,mstahiki meya wa manispaa ya moshi,Zuberi Kidumo na katimu wa ccm wa wilaya.
"Wewe nenda hapo kwenye jengo la ccm wilaya,mtafute fundi anaitwa.........,huuyo atakueleza vizuri maana ndiyo aliyeshuhudia mtia nia akimporomoshea matusi mstahiki meya",amesema mtoa taarifa wetu aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Mmoja wa wajumbe aliyehudhulia kikao hicho hakuwa tayari kuelezea kilichojadiliwa ndani ya kikoa hicho na kuomba atafutwe mwenyekiti wa ccm moshi mjini,faraj Swai mabaye hata hivyo simu yake iliita bila majibu.
Soma Pia: Siasa za kuchafuana zashika kazi CCM Moshi mjini
Nini chanzo cha kada huyo kuvurumisha matusi kwa meya wake,fuatilia ukurasa huu hapo baadae tutaweeka kila kitu.