Mtihani wa Darasa la Saba wafutwa

Binafsi sioni nia ya dhani katika kulikomboa taifa kupitia elimu. Mara zote serikali imekuwa ikiangalia mbinu za kufaulu mitihani kwa takwimu badala ya kutatua matatizo yanayoikumba sekta ya elimu.

Mfano: japo sijaipata na kuisoma kama document, lakini kupitia vyombo vya habari na mitandao nimeona mapungufu yafuatayo; sera haijazungumumzua

1. Malipo ya malimbikizo ya walimu. Huwezi kuwa na sera wakata watekelezaji wa sera wanaidai serikali.

2. Sera imesema kuwa kutakuwa na chombo kinachowaratibu walimu. Je, vipi madai yao ya motivation, kupandishhwa vyeo, kuhama likizo n.k atashughulikia nani?

3. sera inasema juu ya kitabu kumoja cha kufundishia wakati taasisi ya elimu T.I.E ikiwa ina lalamikiwa kwa ubovu wa vitabu vya kiada na EMAC ikiwa inalalamikiwa kwa rushwa na kupitisha vitabu duni vya ziada. sera inapaswa kwanza kushughulikia hawa.

4. Sera inazunugumuzia elimu bure; Je vipi utitiri wa michango wanayotozwa wazazi? mimi nadhani tuangalie mbele; tutatue matatizo ya msingi sio matatizo ya siasa.
 
Wengi mmestuka labda kwa kuwa haijazoeleka itakapofika muda tukaona manufaa yake nadhani hii tension itaisha elimu kwa mfumo wa kiingereza imetufanya tuzalishe wasomi wengi ambao ni mabingwa wa kukariri na sio kuelewa.

Na mi naamini wanafunzi wengi wanafeli cyo km hawasomi tatizo ni lugha kiingereza kwa wengi ni pasua, nadhani kutumia kiswahili kutaongeza ufaulu shuleni.
 
Ni wakati muafaka wa kuondoa utawala huu, mana umetuharibia mambo mengi sana adi elimu mbona hii aibu kubwa sana.
 
Jana mheshimiwa Rais wa Tanzania alizindua Sera mpya ya Elimu ambapo kati ya mengi yaliyomo ndani ya sera hiyo ni kufutwa kwa mtihani wa Darasa la Saba na Elimu ya Msingi kuongezwa hadi Kidato cha Nne.

=========


Source: The Citizen

Hii ndio Tanzania kwa maneno Na vitendo,,sjaelewa chochote
 

kwa vile amesema mpango unatekelezwa kama millenium goal policy.2015-2025. Action should be slightly! Remember that was a launching of tanzania education policy aiming at millenium goal. Kwa upande wa kiswahili siungi mkono ...we needs more than ten years to make swahili a media of instruction rather we wont compete in the word economic,social and political affair .yangu macho!! Kama nitakuwepo majaliwa.!!
 
Mfumo huu wa elimu unakwenda kuzika elimu! Ccm must go!

NI KWELI ELIMU INAZIKWA .IMAGINE .Mpango wa milenia unaanza 2015-2025. Sera inazindukiwa mwaka huo huo ambao mpango wa milenia unaanza.Bila matayarisho sasa mambo yataanzaje mwaka ule ule? Ni kama kukurupuka tu labda kama kuna external pressure!
 

kweli kabisa!
 
tanzania ndo nchi pekee ambayo imebaki kuwa inaiba sera, na matamko ya nchi nyingine kisha kuja kuipaste kwenye mipango yake. ukitaka nenda fuatilia shwala la BRN utakuta ni copy and paste ya malaysia kilichoondolewa ni jina tu kkwamba replace malaysia with tanzania.

sasa kibaya hawakujua wenzao wanayapikaje haya, ndo mana BRN imebaki kuwa bomu litakalolipuka manake wamekula mahela ya kutosha na hakuna kilichofanyika mpaka sasa.

hii sera ya elimu iliyokopiwa itatutia aibu very soon
 
duh hapa kazi ipo maana kiswahili tu chenyewe watu itabidi wakisoma maana pia watanzania wengi hatukifahamu,maneno mengi ya kisayansi yako kwa kiswahili kama yalivyo sidhani kama hapo kitaeleweka kitu dah

mimi naona kutumia kingereza kujifunzia ni rahisi kuliko kutumia kiswahili.kiswahili hakina shortening hambo dogo utazunguka wee! .sentensi kumi za kiswahili zinajibiwa na sentens 3 za kingereza.sikatai kutumia kiswahili lakini inataka maandaluzi sio milenia goal ina range 2015-25 na wewe unaweka sera mwaka ule ule isiyo na maandaluzi.vitabu tu vitawatoa nyongo!!!! Huwa najiuliza viongozi wetu kulikoni!? Hao walimu tu wa sekondari ukiwageuza ghafla kutumia kisw. Umewavuruga!! Mult book system tu imeua kabisa elumu. Waafrika tuna matatizo. Kitendawili?..,tega..au foreigners wanawavuruga viongozi wetu ili warudi kututawala?..licha ya ukoloni mamboleo tulio nao?
 
Yaan majitu mengine bwana sijui ni mabendera tu fuata maupepo. Humuhumu ndo watu walisha lalamika eti mbona nchi za Ulaya zinatumia lugha zao kwenye ufundisaji. pia 90% ya nchi za Africa zina tumia Lugha yao kama the Medium kwny ufundishaji sasa mbona tena mnaongea upuuzi . M naona ni sawa kabisa mia% acheni kuwa mamburula ndo maana nchi inazidi kutawaliwa na mafisadi.
 
ngoja nikae kimya maana povu litanitoka bure. :tape2:
 
Mwl. Sera nyingi za maendeleo katika nchi zinazoendelea, hutengenezwa na mataifa makubwa kupitia taasisi kama WB, na Mashirika yaliyo chini ya mwamvuli wa UN. Mara nyingi huwa ni blueprint kwa maendeleo ya nchi nyingi kwa mfano katika nchi za latini Amerika, Indonesia na hata Afrika nchi kama Angola, Rwanda n.k maendeleo yake yamechagizwa na adoption ya sera hizi.

Tofauti na wao, ambao baada ya kupokea sera hizi kutoka huko kwa "wakubwa" wanazicontextualize na hali halisi ya mifumo, bajeti na rasilimali watu walionazo. sisi kwetu "tunazimeza" nzima-nzima pasipo kuzifanyia critical analysis na tafiti ambazo zitaboresha sera hizo kwa mazingira yetu.
 
Jana mheshimiwa Rais wa Tanzania alizindua Sera mpya ya Elimu ambapo kati ya mengi yaliyomo ndani ya sera hiyo ni kufutwa kwa mtihani wa Darasa la Saba na Elimu ya Msingi kuongezwa hadi Kidato cha Nne.

=========


Source: The Citizen

Elimu yetu kwa kiswahili, wewe unatuwekea post kwa Ki-English, maana yake nini???, Ee Mungu tujalie Uongozi uliopo madarakani utoke mapema, au UFE ili wakae watu wenye kufikiria na kushauri vizuri
 
Jana mheshimiwa Rais wa Tanzania alizindua Sera mpya ya Elimu ambapo kati ya mengi yaliyomo ndani ya sera hiyo ni kufutwa kwa mtihani wa Darasa la Saba na Elimu ya Msingi kuongezwa hadi Kidato cha Nne.

=========


Source: The Citizen
This is OPENLY PROPAGANDA OF POLITICS with lack of Good Strategic Plans.

Kama wameshindwa kuboresha hii TU tulinayo kwa sasa Elimu ya Ngumbaro ya Darasa7 kufaulu PASIPO kujua kusoma,kuandika wala Kuhesabu, Je itawezekana au Mfa Maji haachi kutapatapa.
 
Hi ndo Tanzania nchi yenye udongo wenye dhambi wanalisaka taji la ushindi nasema tanzania biblia nashikilia nawakemea wanaogombania ufalme na umalkia"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…