Mtindo wa ma DC, RC na Mawaziri kusema OCD mchukue huyo wanapozidiwa hoja na wananchi ni wa kitoto sana

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,409
Reaction score
13,262
Kuna matindo wa kitoto, woga, kibabe na kijinga sana sasa hivi unafanywa na ma DC, RC na Mawaziri wakati wakiongea na wananchi wanapozidiwa hoja au wanapotaka wananchi waogope utasikia wanawasukumizia wananchi wanaotoa hoja kwa ma OCD kama mbinu ya kuwanyamazisha.

Hii tabia inajenga hofu kwa wananchi na lengo ni kiwazuia wananchi kuongea. Ukiangalia huwa hakuna kosa lolote mwananchi amefanya lakini ghafla utadisikia, OCD mchukue huyo shughulika naye.

Nitoe wito kwa ma OCD kuwa mkiambiwa wachukueni ninyi kaeni nao pembemi mkutano ukiisha waachieni kwakuwa hawana makosa.

Viongozi acheni woga wapeni nafasi wananchi waongee msiwakatize kutaka waongee kile mkitakacho. Hayo ni mambo ya kizamani sana. Kama mmeshindwa kazi achieni ngazi.
 
Ni ulevi mbaya sana wa madaraka.
By the way tulaumu sheria inayoruhusu hayo, tusilaumu watawala.
 
ni ushamba wa hali ya juu sana, hata ma OCD wenyewe huwa wanawashangaa, it is as if wanaamini wanawamiliki maOCD. yetu kuna siku na wao hao hao huwa wanakuja kukunjwa na maocd.
 
Inaonyesha ni jinsi gani kuna hole kwenye katiba na sheria za nchi, nchi zingine hakuna such thing, is why katiba mpya need reforms
 
Ninachoamini hii nchi watawala wasipojirekebisha iko siku kitanuka. Haijalishi itachukua muda gani niwe hai ama nimekufa ila hii nchi kwa mwendo tunaoenda nao siku moja tutaitafuta amani kwa tochi kama Kenya.

Waendesha V8 wanajisahau sana, wanashiba mpaka wanakuwa na dharau kwa watu wengine
 
Ni wapumbavu sana Hawa!
 
M
Mchukue huyu🤣🤣🤣
 
Dawa wakuu wa mikoa wapigiwe kura, wataacha huo ujinga
 
Hawasomi historia, hawakumbuki kilichomtokea Kleruu. Viongozi hawataki Changamoto mfano ni yule mkuu wa mkoa wa Dar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…