Mnamo tarehe 4/8/2014 ndugu Gaden Mhagama mkazi wa Ilinida,Ludewa ametiwa hatiani kwa makosa mawili ya kushawishi kutoa rushwa 30,000 na kutoa rushwa 50,000 kwa askari polisi koplo Samson Hango.
Mwendesha mashitaka wa Takukuru ndg Frednand Nsakuzi alidai mahakamani kuwa mtuhumiwa alitenda makosa hayo ndani ya mwezi Julai 2013 huko Ikonda,wilayani Makete mkoani njombe na hivyo kuhukumiwa kifungo cha miaka mitatu kwa kila kosa ama faini ya 500,000/=kwa kila kosa hukumu iliyotolewa na mh.Lyakinana