JOKE.
Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 9 alikuwa anahitaji sana shilingi 100,000 (laki moja). Akamuuliza mama yake ni jinsi gani anaweza kupata pesa hizo. Mama yake akamwambia "muombe Mungu atakupatia. Mtoto alianza kuomba kila siku na kila mara lakini hakupata hiyo pesa toka kwa Mungu. Hatimaye akafikia uamuzi wa kumuandikia barua Mungu ili asome maombi yake. Kisha akai-post barua ile. Wakati wafanyakazi wa posta wakichambua barua kwa ajili ya kuzipeleka sehemu husika, walishangazwa kuona bahasha iliyoandikwa "Kwa Mwenyezi Mungu" na wakashindwa kuelewa mahali
pa kuipeleka, Wakaamua kuifungua.
Barua ilisomeka hivi:
"Mpendwa Mungu,
Jina langu ni EMMANUELEY, nina umri wa miaka 9 na ninasoma darasa la
tatu katika jiji la Dar es salaam ambalo liko katika nchi ya Tanzania ,
bara la Africa .
Nimeamua kukuandikia barua hii kukuomba kiasi cha shilingi laki moja
baada ya kuomba bila kupata majibu toka kwako.
Naomba sana unisaidie kwani mimi ni mtoto mdogo na sina uwezo wa kufanya kazi na kupata pesa. Pia wazazi wangu hawana uwezo kwani hata nchi yetu
ni maskini sana .
Natanguliza shukrani.
Wako mtiifu,
EMMA."
Wafanyakazi wa posta walifurahishwa sana na barua hiyo na kisha wakaamua
waipeleke kwa Rais KIKWETE. Rais KIKWETE naye alipoipokea ilimfurahisha
sana na kisha akamwambia Secretary wake achukue sh. 2000 amtumie mtoto
huyo akidhani kuwa pesa hizo ataziona kuwa nyingi sana .
Mtoto huyo alipopokea hizo shilingi 2000 alijibu hivi:
"Mpendwa Mungu wangu,
Nashukuru sana kwa kusikiliza maombi yangu na kunitumia pesa nilizokuomba. Lakini nimebaini kuwa uliamua kuzituma kupitia serikali yetu ya Tanzania . Kama ilivyo kawaida yao hao wezi, wamekata kiasi cha sh. 98,000 kwa ajili ya kodi , kwa hiyo wameniletea Sh. 2000 tu
Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka 9 alikuwa anahitaji sana shilingi 100,000 (laki moja). Akamuuliza mama yake ni jinsi gani anaweza kupata pesa hizo. Mama yake akamwambia "muombe Mungu atakupatia. Mtoto alianza kuomba kila siku na kila mara lakini hakupata hiyo pesa toka kwa Mungu. Hatimaye akafikia uamuzi wa kumuandikia barua Mungu ili asome maombi yake. Kisha akai-post barua ile. Wakati wafanyakazi wa posta wakichambua barua kwa ajili ya kuzipeleka sehemu husika, walishangazwa kuona bahasha iliyoandikwa "Kwa Mwenyezi Mungu" na wakashindwa kuelewa mahali
pa kuipeleka, Wakaamua kuifungua.
Barua ilisomeka hivi:
"Mpendwa Mungu,
Jina langu ni EMMANUELEY, nina umri wa miaka 9 na ninasoma darasa la
tatu katika jiji la Dar es salaam ambalo liko katika nchi ya Tanzania ,
bara la Africa .
Nimeamua kukuandikia barua hii kukuomba kiasi cha shilingi laki moja
baada ya kuomba bila kupata majibu toka kwako.
Naomba sana unisaidie kwani mimi ni mtoto mdogo na sina uwezo wa kufanya kazi na kupata pesa. Pia wazazi wangu hawana uwezo kwani hata nchi yetu
ni maskini sana .
Natanguliza shukrani.
Wako mtiifu,
EMMA."
Wafanyakazi wa posta walifurahishwa sana na barua hiyo na kisha wakaamua
waipeleke kwa Rais KIKWETE. Rais KIKWETE naye alipoipokea ilimfurahisha
sana na kisha akamwambia Secretary wake achukue sh. 2000 amtumie mtoto
huyo akidhani kuwa pesa hizo ataziona kuwa nyingi sana .
Mtoto huyo alipopokea hizo shilingi 2000 alijibu hivi:
"Mpendwa Mungu wangu,
Nashukuru sana kwa kusikiliza maombi yangu na kunitumia pesa nilizokuomba. Lakini nimebaini kuwa uliamua kuzituma kupitia serikali yetu ya Tanzania . Kama ilivyo kawaida yao hao wezi, wamekata kiasi cha sh. 98,000 kwa ajili ya kodi , kwa hiyo wameniletea Sh. 2000 tu