Mtoto amefia tumboni akiwa na miezi saba, je haya maelezo niliyo pewa hospital ni sahihi na ni bora kwa afya!?

Poleni Sana.
Inaonekana sheria zinatofautiana, maana kama nchi nyingine wanaweka maslahi ya mzazi/mama mbele zaidi.

Nikuvumilia tu, ila anahitaji uangalifu wa karibu kutoka kwa mume na ndugu....

Asije kukutana na wasiojua wakamuuliza....eehh naona tumbo linazidi kukua, hongera lini unatuletea mtoto?
Hii kauli inaumiza na anaweza kukosa jibu lakumpa mtu inategemea mko na ukaribu upi.

Mungu amtangulie amalize hiyo safari salama na ampe nguvu na afya ya kujaribu tena kubeba ujauzito.
Hawakutoa Option, maelezo niliyo toa ndio tuliyopewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo labda ni utaratibu wa hospital za serikali nchini tu!
Kwa hospitali za binafsi mara tu baada ya kujua hali hiyo wangemshauri wakitoe mara moja!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inaogopesha kama hospitali ndani ya nchi Moja...zinakuwa na utaratibu tofauti juu ya afya ya mgonjwa....
Najua ni utaratibu ulikuwepo mda, ila baadhi ya nchi umeanza kubadilisha hizi taratibu, kama sikosei Israeli ni mojawapo...

Ni bora mama angekuwa hajui ikamtokea akipata uchungu akajifungua nakugundua hivyo kuliko kumwacha aendelee kuteseka kiakili na baadae aanze upya kuugulia maumivu baada ya maziko...

Nikwavile sio jambo linalotokeaaga kila mara ndio maana hatusikii wanawake/familia wakilalamika.
Huo labda ni utaratibu wa hospital za serikali nchini tu!
Kwa hospitali za binafsi mara tu baada ya kujua hali hiyo wangemshauri wakitoe mara moja!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kimsingi kiumbe tumboni huwa hakiozi haraka na hizo 14 inawezekana ila kama itashindikana itabid wamuongeze uxhumgu kwa njia ya dawa ila pia wanaweza mfanyia c section yote kunusuru hari ya mama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amina

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Government hospital bila shaka
 
Mmm ni kumtesa tuu..
Kunabndugu yangu mkewe ilitokea kama huyuhuyu walipogundua mumewe na baadhi ya ndugu waliambiwa yule mjamzito alichomwa sindano hata nusu saa haijaisha uchungu ulimjaa akazaa na tukaenda kuzika siku ile ile.
 
Watu humu wanaona ushauri huu kwa hisia umetoka hospitali ya serikali kwa nadharia ya kwamba hawajali.

Ila kuna vitu vingi vinafanyika hospitali za binafsi si kwa maslahi ya mgonjwa bali kwa maslahi ya hospitali.

Na kwa sababu wengi tunaaminishwa hivyo tunaamini huko ndiko salama, si kweli.

Hilo jambo la kawaida kusubiri.
Kwa sababu akianzishiwa uchungu ikaleta shida inabidi azalishwe kwa operation kitu ambacho ni shida kubwa katika sura zote.

Ukianza wenyewe chance za kujifungua bila shida ni kubwa zaidi ingawaje vyote vinawezekana.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe ungekuwa mama ungejisikiaje kubebelea kiumbe mfu kwa wiki mbili?
Binafsi nisingeweza

Hospital wangempa options zikiambatana na sababu za kila option
Mama atachagua mwenyewe!

Kwa hiyo hospital ikishakuwa ni ya serikali basi daktari ndiye msemaji wa mwisho
 
Fanya fasta wakaichomoe kabla mama mjamzito hajapata infections, fasta yaani. Huyo doctor inabidi achukuliwe hatua kwa kuhatarisha maisha ya mama mjamzito, yaani mtoto aendelee kuoza tu huku mama akisubiri.
 
Ni kweli kupewa option ni jambo muhimu. Mara nyingi nafasi ipo. Lakini si mara zote huleta matokeo chanya.
Nawajua wengi walokufa kwa kukataa ushauri wa daktari. Nawajua wengi ambao walienda fanya ndivyo sivyo baadaye. Nawajua pia waliopotoshwa.

Humu kuna wengi professional wameshauri kuwa asubirie. Maana yake utaratibu huu ni bora zaidi kwa mama kwa ujumla wake kitiba. Madhara ya kisaikolojia na kimwili huzingatiwa wakati hizi taratibu zinakubaliwa. Pia hali ya mama, ukubwa na umri wa kiumbe unazingatiwa.
Inawezekana baadaye liwe jambo la ajabu lakini kwa sasa kwa mazingira yetu ya tiba ni salama zaidi.

Kuhusu kuweza, nikuhakikishie tu ni wengi wanaweza kuliko wanaoshindwa. Hata hivyo huambiwa wakiona hali tofauti warudi hospitali. Milango iko wazi kama anajisikia tofauti.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…